Monday, May 22, 2017

RAMAPHOSA ATAHADHARISHA AFRIKA KUSINI KUGEUKA NCHI YA KIMAFIA

Makamu wa Rais wa Afrika Kusini ametahadharisha juu ya nchi hiyo kugeuka na kuwa ya Kimafia.
Cyril Ramaphosa Makamu wa Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini sambamba na kumkosoa Zuma amesisitiza kuwa, kama chama tawala wa ANC kinataka kisipoteze himaya na udhibiti wa jamii ya nchi hiyo, basi hakipaswi kuruhusu Afrika Kusini igeuke na kuwa nchi ya Kimafia.
Makamu huyo wa Rais wa Afrika Kusini anayetajwa kama mrithi wa Rais Zuma katika uchaguzi ujao, ametoa wito wa kuweko uchunguzi huru kuhusiana na faili la ufisadi ambalo limewatia katika alama ya swali baadhi ya viongozi wa ngazi za juu wa nchi hiyo.
Maandamano dhidi ya  Rais Zuma yamekuwa yakifanyika mara kwa mara nchini Afrika Kusini
Chama tawala nchini Afrika Kusini katika miaka ya hivi karibuni kimepungua umaarufu wake kutokana na viongozi wa ngazi za juu wa chama hicho akiwemo Rais Jacob Zuma kukabiliwa na tuhuma mbalimbali zikiwemo za ufisadi na utovu wa maadili.
Disemba mwaka huu chama hicho kinatarajiwa kumtangaza mrithi wa Rais Jacob Zuma anayemaliza muda wake ambapo Cyril Ramaphosa, Makamu wa Rais wa nchi hiyo amekuwa akitajwa kama chaguo la chama hicho katika uchaguzi ujao uliopangwa kufanyika nchini humo mwaka 2019.

No comments:

Post a Comment