Sunday, March 26, 2017

WENGI WAJITOKEZA KATIKA UCHAGUZI WA SAARLAND UJERUMANI KULIKO 2012

Idadi ya Wajerumani waliojitokeza kupiga kura katika uchaguzi wa jimbo dogo la magharibi la Saarland ni juu kidogo kuliko idadi ya waliojitokeza katika uchaguzi uliopita wa mwaka 2012. Hadi kufikia saa nane mchana wa leo takriban asilimia 32.6 ya wapiga kura walishapiga kura zao, tofauti na uchaguzi uliopita ambapo wakati sawa na huo, ni asilimia 31.1 ya wapiga kura ndio walikuwa wamejitokeza. Ongezeko la asilimia hiyo ndogo inatizamwa kuwa ishara za awali ya jinsi hali itakavyokuwa katika uchaguzi mkuu wa Ujerumani mwezi Septemba. Uchaguzi huo unaojiri miezi sita kabla ya uchaguzi mkuu mwezi Septemba, unatizamwa kama kipimo kinachoweza kubaini ushawishi wa Kansela Angela Merkel dhidi ya washindani wake wa siasa za wastani za mrengo wa kushoto. Uchaguzi huo ni wa kwanza miongoni mwa chaguzi tatu za majimbo zitakazofanyika kabla ya uchaguzi mkuu. Kadhalika ndio uchaguzi wa kwanza tangu Martin Schulz kuidhinishwa na chama chake cha SPD kugombea ukansela dhidi ya Merkel.

No comments:

Post a Comment