Sunday, March 26, 2017

HRW YATAKA RAIS WA SUDSN SZUIWE KUINGIS JORDDN AU AKAMATWE

Shirika la kimataifa la Haki za Binadamu HRW limetaka Rais Omar al Bashir wa Sudan azuiwe kuingia nchini Jordan.
Kwa mujibu wa shirika la habari la AFP, Human Rights Watch imetoa tamko la kuitaka serikali ya Jordan imma imzuie Rais Omar al Bashir kutembele nchi hiyo au imtie mbaroni mara atakapowasili nchini humo.
Taasisi hiyo ya kimataifa isiyo ya kiserikali imegusia tuhuma zinazomkabili Rais wa Sudan za kuhusika katika jinai za kivita za jimbo la Darfur la magharibi mwa nchi hiyo na kuitaka serikali ya Jordan iheshimu makubaliano ya kimataifa.
Katika tamko lake hilo Human Rights Watch imesema, kwa vile Jordan ni mwanachama wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC, ina wajibu wa kutekeleza makubaliano yaliyounda mahakama hiyo. Shirika hilo la haki za binadamu limedai pia kuwa, kama Jordan itamruhusu Rais al Bashir kutembelea nchi hiyo au kama haitomtia mbaroni, itakuwa imekwenda kinyume na ahadi zake kwa mujibu wa makubaliano ya ICC. 
Mahakama ya ICC inadai kuwa Rais Omar al Bashir wa Sudan amehusika katika jinai za kivita katika jimbo la Darfur na imetoa waranti wa kutiwa mbaroni.
Kikao cha wakuu wa Jumuia ya Nchi za Kiarabu kimepangwa kufanyika Jumatano ya tarehe 29 mwezi huu wa Machi nchini Jordan. Rais Omar al Bashir amealikwa kushiriki kwenye kikao hicho.
Jimbo la Darfur la magharibi mwa Sudan lilikumbwa na machafuko tangu mwaka 2003 kulalamikia kudharauliwa na kutelekezwa na serikali.

No comments:

Post a Comment