Sunday, March 26, 2017

MAGAIDI WATANO WAUAWA , 16 WATIWA MBARONI KASKAZINI MWA MISRI

Wanajeshi wa Misri katika operesheni ya kupambana na mgaidi, Sinai Kaskazini
Jeshi la Misri leo limetoa taarifa na kusema kuwa, limefanikiwa kuua magaidi watano na kuwatia mbaroni wengine 16 katika operesheni maalumu iliyofanywa na jeshi hilo kaskazini mwa Misri.
Msemaji wa jeshi la Misri, Kanali Tamer el  Refae amesema, magaidi watano wakufurishaji akiwem mmoja wa viongozi wa kundi la kigaidi Baytul Muqaddas linalofanya mashambulizi yake mengi kaskazini mwa Rasi ya Sinai wameuawa kwenye operesheni hiyo. Amesema, magaidi wengine 16 wametiwa mbaroni katika opereseheni hiyo.
Kwa mujibu wa Kanali Tamer el Refae, jeshi la Misri limekamata pia kiwango kikubwa cha silaha pamoja na kutegua mabomu yaliyokuwa yametegwa na wanamgambo hao.
Magaidi wa Daesh wakijiandaa kushambulia makazi ya raia kwa roketi wanaloliita "Jahannam"

Eneo la Sinai Kaskazini huko Misri limeshuhudia mashambulizi mengi ya kigaidi tangu mwaka 2013 baada ya jeshi la nchi hiyo kufanya mapinduzi yaliyoongozwa na Rais wa hivi sasa wa Misri, Jenerali Abdul Fattah el Sisi. Mapinduzi hayo ya kijeshi yalimuondoa marakani rais wa kwanza kuchaguliwa kidemokrasia nchini Misri, Mohammad Morsi ambaye hivi sasa yuko jela. Al Arish ambayo ndiyo makao makuu ya mkoa huo wa kaskazini mwa Misri ndio mji unaoshuhudia mashambulizi mengi ya kigaidi.
Hadi hivi sasa kundi la Ansar Baytul Muqaddas limeshafanya makumi ya mashambulizi dhidi ya maeneo ya wanajeshi na raia wa kawaida wa Misri na kuua watu wengi sambamba na kuharibu miundombinu ya nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika.

No comments:

Post a Comment