Friday, March 30, 2018

POLISI TANZANIA: HATUJABAINI SILAHA ILIYOTUMIKA KUMUUA AKWILIN, LEMA ASHANGAA

Polisi Tanzania:  Hatujabaini silaha iliyotumika kumuua Akwilina, Lema ashangaa
Kamanda wa jeshi la polisi kanda maalum ya Dar es Salaam nchini Tanzania, Lazaro Mambosasa, amesema kuwa hadi sasa bado jeshi hilo linaendelea na uchunguzi kuhusu tukio la kuuawa kwa kupigwa risasi mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwilini.
Hata hivyo Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema ameshangazwa na taarifa hiyo iliyotolewa na Kamanda wa kanda maalumu ya Dar es Salaam Lazaro Mambosasa kuhusu kutojulikana silaha iliyotumika kumuua Akwilina na kuandika katika ukurasa wake wa Twitter kwamba: “Nimeitafakari kauli ya Mambosasa inayohusu tukio la Akwilini kuhusu silaha iliyotumika, bila shaka kuna dhambi kubwa inapangwa nawasihi Wana CHADEMA kuwa makini wakati huu kwani si ajabu ukasikia kuwa Ile silaha iliyotumika kumuua Akwilini imekutwa nyumbani kwa Kiongozi wa CHADEMA” -Lema

Kamanda wa jeshi la polisi kanda maalum ya Dar es Salaam Lazaro Mambosasa alisema jana Ijumaa mbele ya waandishi wa habari bado hawajabaini ni silaha gani ilitumika katika tukio la mauaji ya Akwilina Akwini, ambaye kifo chake kimezusha malalamiko makubwa ya asasi mbalimbali na kiraia nchini Tanzania.
Akwilina Akwilini, mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT)
“Bado tunaendelea na upelelezi wa tukio hili. Hatujajua ile silaha iliyotumika hadi kumpata Akwilina kwa sababu askari walikuwa wengi siku ile na hakukuwa na ushahidi ni yupi aliyetenda kosa hilo.“ Amesema Mambosasa. Hii ni katika hali ambayo, tarehe 18 Februari mwaka huu Kamanda Lazaro Mambosasa alinukuliwa akisema kuwa, jeshi la polisi linawashikilia askari wake sita na silaha zao kwa ajili ya uchunguzi zaidi kuhusiana na tukio hilo.
Polisi wakituliza ghasia nchini Tanzania
Akwilina Akwilini, aliuawa kwa kupigwa risasi tarehe 16 Februari mwaka huu, wakati polisi walipokuwa wakiwatawanya wafuasi wa chama cha upinzani cha Demokrasia na Maendelea (CHADEMA) waliokuwa wanaamdamana kuelekea ofisi za mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni kushinikiza mawakala wao kupatiwa barua za viapo vyao kwa ajili ya kusimamia uchaguzi mdogo uliopita wa jimbo hilo.

No comments:

Post a Comment