Friday, March 2, 2018

AL-SHABAAB YAUA ASKARI 5 WA KENYA KAUNTI YA MANDERA

Al-Shabaab yaua askari polisi 5 wa Kenya kaunti ya Mandera
Askari polisi watano wa Kenya wameuawa na wengine watatu kujeruhiwa baada ya wanachama wa kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab kushambulia kambi mbili za maafisa usalama katika mji wa Fino katika kaunti ya Mandera.
Naibu Kamishna wa kaunti ndogo ya Laafey huko kaskazini mwa Kenya, Eric Oronyi amesema shambulizi hilo limefanyika usiku wa kuamkia leo, ambapo wanamgambo hao wamevamia kituo cha polisi wa kawaida na wa utawala katika mji wa Fino.
Amesema wavamizi hao kati ya 70 hadi 100 mbali na kutekeleza mauaji hayo, kadhalika wameng'oa mlingoti wa shirika moja la simu za rununu na kulemaza mawasiliano.
Magaidi hao wamekuwa wakishambulia mabasi ya uchukuzi wa umma kaunti ya Mandera na kuua
Mwezi uliopita, maafisa wengine watano wa polisi ya Kenya waliuawa baada ya wanachama wa al-Shabaab kushambulia msafara wa magari ya maafisa usalama katika barabara ya Elwak-Kotulo katika kaunti hiyo hiyo ya Mandera.
Kundi la kigaidi la al-Shabaab lenye makao yake Somalia mara kwa mara hutekeleza mashambulizi ndani ya ardhi ya Kenya kuishinikiza serikali ya nchi hiyo iondoe wanajeshi wake wanaohudumu katika Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Afrika Somalia, AMISOM

No comments:

Post a Comment