Sunday, March 25, 2018

RAIS WA IRAN LEO ANAELEKEA TURKMENISTAN NA JAMUHURI YA AZERBAIJAN

Rais wa Iran leo anaelekea Turkmenistan na Jamhuri ya Azerbaijan
Rais Hassan Rouhani wa Iran leo anaanza safari ya siku mbili ya kuzitembelea nchi jirani za Turkmenistan na Jamhuri ya Azerbaijan kwa lengo la kujadiliana na viongozi wa nchi hizo uhusiano wa pande mbili na matukio ya hivi karibuni ya kieneo.
Akiongoza ujumbe wa ngazi za juu, Rais Rouhani ataelekea Ashgabat, mji mkuu wa Turkmenistan katika duru ya kwanza ya safari yake kufuatia mwaliko wa rais mwenzake wa nchi hiyo Gurbanguly Berdimuhamedow.
Kwa mujibu wa Parviz Ismaili,  mkuu wa kitengo cha habari katika Ofisi ya Rais wa Iran, katika safari hiyo nchi hizo mbili zitatiliana saini mikataba kadhaa ya ushirikiano hasa katika sekta za biashara. Marais Aliyev wa Jamhuri ya Azerbaijan (kushoto) na Rouhani wa Iran katika mkutano wao mjini Tehran mwaka jana
Aidha akiwa Turkmenistan, Rais Rouhani atatembelea mji wa kale wa Merv siku ya Jumatano. Baada ya hapo Rouhani ataelekea Baku, mji mkuu wa Jamhuri ya Azerbaijan ambapo atafanya mazungumzo na rais wa nchi hiyo Ilham Aliyev. Inatazamiwa pia katika safari hiyo nchi mbili zitatiliana saini mikataba kadhaa ya ushirkiano wa kiuchumi.

No comments:

Post a Comment