Friday, February 2, 2018

MTOTO MKUBWA WA FIDEL CASTRO AJIUA CUBA, MSONGO WA MAWAZO WATAJWA KUWA CHANZO

Mtoto mkubwa wa Fidel Castro ajiua Cuba, msongo wa mawazo watajwa kuwa chanzo
Mtoto mkubwa wa aliyekuwa rais wa Cuba, Fidel Castro, Fidel Ángel Castro Díaz-Balart mwenye umri wa miakka 68 jana alikutwa amejiua huko Havana, mji mkuu wa nchi hiyo.
Castro Díaz-Balart aliyefahamika kwa jina maarufu la Fidelito ametajwa na madaktari kwamba alikuwa ana matatizo ya msongo wa mawazo. Kabla ya hapo Fidelito alikuwa mshauri wa kisayansi wa Baraza la Serikali ya Cuba na alifanya kazi kama Makamu wa Rais wa Chuo Kikuu cha Sayansi nchini Cuba, huku akiwa pia mwanafizikia wa nyuklia nchini humo.
Castro Díaz-Balart, enzi za uhai wake
Gazeti rasmi la Serikali ya Cuba la Granma limeripoti kuwa; “Fidel Castro Diaz-Balart, alikuwa akipatiwa matibabu na kundi la madaktari kwa miezi kadhaa kutokana na msongo wa mawazo, ambao unatajwa kuwa chanzo cha yeye kujitoa uhai. Televisheni ya taifa ya nchi hiyo imetangaza kwamba, mtoto huyo wa aliyekuwa rais wa kwanza wa nchi hiyo alikuwa akipata matibabu katika miezi ya hivi karibuni kama mgonjwa wa kutibiwa na kurudi nyumbani, baada ya kulazwa hospitalini kwa muda. Baba yake, Mzee Fidel Castro, alifariki dunia mwezi November 2016 akiwa na umri wa miaka 90 baada ya kuugua kwa muda mrefu.

No comments:

Post a Comment