Saturday, February 24, 2018

BARAZA LA USALAMA LA UN LAPASISHA AZIMIO LA KUSITISHA VIATA KWA SIKU 30 SYRIA

Baraza la Usalama la UN lapasisha azimio la kusitisha vita kwa siku 30 Syria
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limepasisha azimio la kusitishwa vita kwa siku 30 nchini Syria na kuruhusu upelekaji wa misaada ya kibinadamu katika maeneo yanayozingirwa.
Azimio hilo ambalo limepasishwa na wanachama wote 15 wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeyaondoa makundi ya kigaidi chini ya mwavuli wa uamuzi huo wa kimataifa kutokana na msimamo imara wa Russia.
Kwa mujibu wa azimio hilo, misaada ya kibinadamu itaanza kutumwa mara moja katika maeneo yote yanayozingirwa nchini Syria hususan eneo la Ghouta Mashariki. Eneo hilo la kistratijia lililoko karibu na mji mkuu wa Syria, Damascus, linadhibitiwa na makundi ya kigaidi yanayoungwa mkono na Marekani, Saudi Arabia na washirika wao, na serikali ya Rais Bashar Assad inafanya jitihada za kulikomboa na kuwafurusha magaidi katika eneo hilo. 
Magaidi hao wamekuwa wakitumia eneo hilo la Ghuota Mashariki kushambulia mji mkuu wa Syria kwa maroketi karibu kila siku na kuua raia wasio na hatia. 
Vasily Nebenzya
Baada ya kupasishwa azimio hilo balozi na mwakilishi wa Russia katika Umoja wa Mataifa, Vasily Nebenzya amekosoa sera za kibeberu za muungano unaoongozwa na Marekani huko Syria na kusema, makundi ya waasi yanayosaidiwa na muungano huo ndiyo yanayohusika na mgogoro wa kibinadamu katika eneo la Ghuota Mashariki.
Nebenzya pia amekosoa propaganda chafu zinazofanywa na vyombo vya habari vya nchi za Magharibi dhidi ya majeshi ya serikali ya Syria katika mapigano ya sasa huko Ghuota Mashariki. 

No comments:

Post a Comment