Saturday, February 10, 2018

MAMILIONI YA WAIRAN LEO KUSHIRIKI KATIKA KILELE CHA SHEREHE ZA MAPINDUZI YA KIISLAMU

Mamilioni ya Wairan leo kushiriki katika kilele cha sherehe za Mapinduzi ya Kiislamu
Mamilioni ya Wairan muda mchache kutokea hivi sasa watamiminika mabarabarani kwa ajili ya kushiriki katika kilele cha sherehe za miaka 39 ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu humu nchini.
Hii ni katika hali ambayo maraajii wa kidini na viongozi mbalimbali wa kisiasa wamewataka wananchi wa Iran kushiriki kwa umoja na kwa wingi katika maandamano hayo ya mamilioni ya watu katika miji yote ya nchi hii. Mjini Tehran maandamano hayo yatahudhuriwa na Rais Hassan Rouhani ambaye kama kawaida atatoa hotuba katika uwanja wa Azad katikati mwa mji wa Tehran, kama ambavyo pia watahudhuria viongozi wa ngazi mbalimbali wa serikali.
Kilele cha ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran
Sherehe za ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran huadhimishwa tarehe 22 Bahman kila mwaka sawa na tarehe 11 Februari, ambazo hukumbushia siku muhimu ambayo Imam Ruhullah Musawi Khomein alirejea kutoka uhamishoni na kisha kutangaza kuunda serikali mpya inayoungwa mkono na wananchi tofauti na ile iliyokuwepo wakati huo ambayo ilikuwa ni kibaraka wa Marekani, madola ya Magharibi na utawala haramu wa Kizayuni wa Israel.
Hata hivyo suala la kufaa kuzingatiwa ni kwamba, tangu Iran ilipojitangazia mfumo wa Kiislamu nchini hapa, madola ya Magharibi yakiongozwa na Marekani na washirika wao wamekuwa wakifanya njama za kila namna ikiwemo vikwazo vya kila upande kwa lengo la kuipigisha magoti Iran ya Kiislamu, suala ambalo hata hivyo limeendelea kugonga mwamba kwa kipindi chote cha tangu kupata ushindi Mapinduzi ya Kiislamu na kuundwa mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.

No comments:

Post a Comment