Thursday, April 12, 2018

WANARIADHA 13 WA AFRIKA ' WATOWEKA' AUSTRALIA

Wanariadha 13 wa Afrika 'watoweka' Australia
Wanariadha 13 wa Afrika walioenda kushiriki Michezo ya Jumuiya ya Madola nchini Australia wametoweka katika mazingira ya kutatanisha.
David Grevemberg, Afisa Mkuu Mtendaji wa Shirikisho la Michezo ya Jumuiya ya Madola amewaambia waandishi wa habari leo Alkhamisi mjini Gold Coast kunakofanyika mashindano hayo kuwa: "Wanariadha wengine watano raia wa Rwanda, Uganda na Sierra Leone wametoweka na kwenda kusikojulikana."
Ameongeza kuwa, hii ni baada ya wanariadha wengine wanane kutoka Cameroon kutoweka hapo awali, na sasa idadi hiyo ya wanaichezo wa Kiafrika waliotoweka katika mazingira ya kutatanisha nchini humo imefikia 13.
Serikali ya Australia imetoa viza kwa wanamichezo wanaoshiriki katika michezo hiyo, kuendelea kuwa nchini humo hadi tarehe 15 mwezi Mei. 
Wakimbizi kutoka nchi mbalimbali duniani huko Australia
Peter Dutton, Waziri wa Masuala ya Ndani ya Australia ameonya kuwa, mwanariadha yeyote atakayebaki nchini humo kinyume cha sheria baada ya muda wake wa viza kumalizika, atafurushwa nchini humo kwa nguvu.
Ni vyema kukumbusha hapa kuwa, mwaka 2000 wakati wa mashindano mengine ya Jumuiya ya Madola jijini Sydney, wanaridha zaidi ya 100 waliendelea kuishi katika jiji hilo hata baada ya kumalizika kwa michezo hiyo.

No comments:

Post a Comment