Thursday, April 12, 2018

KREMLIN YAJIBU TWITTER YA TRUMP: MAKOMBORA EREVU YANAPASWA KUELEKEZWA KWA MAGAIDI, SI KWA SERIKALI HALALI

Kremlin yajibu Twitter ya Trump: Makombora erevu yanapaswa kuelekezwa kwa magaidi, si kwa serikali halali
Msemaji wa Ikulu ya Rais wa Russia, Kremlin amesema Moscow Russia haishiriki katika udiplomasia wa Twitter.
Dimitri Peskov ameyasema hayo akijibu ujumbe ulioandikwa na Rais Donald Trump wa Marekani katika mtandao wa kijamii wa Twitter ambaye ameitahadharisha Russia kwamba isubiri makombora ya Marekani huko Syria.  
Peskov amesema kuwa, Russia inaunga mkono hatua madhubuti na inaamini kuwa ni muhimu kujiepusha na hatua yoyote inayoweza kuchafua zaidi hali iliyopo hivi sasa.
Mapema leo Rais Donald Trump wa Marekani aliimbia Russia kupitia mtandao wa Twitter kwamba ijitayarishe kwa mashambulizi ya makombora "mazuri, mapya na erevu" huko Syria. Marekani inadai serikali ya Syria imetumia silaha za gesi ya sumu katika eneo la Douma huko Ghuta Mashariki, suala linalokadhibishwa na Syria na Russia. 
Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya kigeni ya Russia, Maria Zakharova pia amejibu matamshi hayo akisema: Mashambulizi erevu yanapaswa kuelekezwa kwa magaidi ni si kwa serikali halali ya Syria.
Image Caption
Russia pia imesema kuwa itayatungua makombora yote ya Marekani yatakayopigwa kueleka Syria na kwamba itapiga mahala yatakakotokea.

No comments:

Post a Comment