Friday, April 13, 2018

AYATULLAH AKHTARI: MAWAHABI WANAPIGWA NA WANAZUONI NA MATAIFA YA KIISLAMU

Ayatullah Akhtari: Mawahabi wanapingwa na wanazuoni na mataifa ya Kiislamu
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimatataifa ya Ahlul-Beit (AS) amesisitiza kuwa, utawala wa Aal Saud hauna nafasi yoyote si ya kielimu wala uungaji mkono wa wananchi na kwamba, akthari ya wanazuoni wa Kiislamu wanawapinga Mawahabi wa Saudi Arabia.
Ayatullah Muhammad Hassan Akhtari amesema hayo akiwa nchini Syria na kubainisha kwamba, Maulama waliowengi wa Kiislamu na mataifa ya Kiislamu wanachukia Uwahabi ulioletwa na Aal Saud.
Ayatullah Akhtari ameongeza kuwa, aidiolojia ya uchupaji mipaka ya Uwahabi ambayo inaenezwa na kuungwa mkono na Saudi Arabia imepelekea kutokea magaidi ambao wamekuwa wakifanya mashambulio ya kigaidi katika maeneo mbalimbali ulimwenguni.
Katibu Mkuu wa Jumuiya yay Kimataifa ya Ahlul-Beit (AS) amesema Saudia inataka kulinda nafasi yake kupitia kuzusha hitilafu na mifarakano pamoja na kutekeleza mauaji dhidi ya raia wasio na hatia.
Uwahabi
Aidha ameashiria juhudi za utawala wa Saudi Arabia za kutaka kuwa na uhusiano wa kawaida na utawala haramu wa Israel na kusema kuwa, hatua hiyo ya utawala wa Riyadh inalenga kuulinda na kuuhifadhi utawala huo, hata hivyo jambo hilo linalaaniwa na Waislamu ulimwenguni.
Kadhalika Katibu Mkuu wa Jumuiya yay Kimataifa ya Ahlul-Beit (AS) amesema kuwa, Saudia imeamua kuuunga mkono utawala dhalimu wa Israel ili kuifurahisha Marekani.
Ayatullah Akhtari ameashiria pia kwamba, watawala wa Saudia wamebomoa athari nyingi za Kiislamu katika miji mitakatifu ya Makka na Madina na kuongeza kwamba, wanachofuatilia Aal Saud ni kuzusha fitina na mifarakano miongoni mwa Waislamu.

No comments:

Post a Comment