Sunday, April 8, 2018

RASMI ALIYEKUWA RAIS WA BRAZIL AJISALIMISHA TAYARI KUTUMUIKIA KIFUNGO

Rais wa zamani wa Brazil Luiz Inacio Lula da Silva amewasili katika jela la Curibita kuanza kutumikia kifungo cha miaka 12 jela.
Hatua hiyo ya kujisalimisha kwa polisi ameichukua baada ya mahakama siku ya Ijumaa kumhukumu kwa mashitaka ya ufisadi. Matangazo ya moja kwa moja ya vituo vya televisheni vya Brazil yameonesha akiwasili kwa helikopta katika makao makuu ya polisi katika mji wa Curibita ulioko kusini mwa Brazil.
Mwanasiasa huyo mwenye umri wa miaka 72 aliondoka Sao Paoli akiwa amezingirwa na walinzi kwenye jengo la muungano wa wafuaji vyuma mjini humo. Alipenya katikati ya wafuasi wake waliokuwa wanamzuia asiondoke na kuingia katika gari la polisi. Anasisitiza kuwa mashitaka dhidi yake yalichochewa kisiasa. Lula alikutwa na hatia ya kupokea rushwa kutoka kwenye kampuni kubwa ya ujenzi, ili iweze kupata mikataba ya serikali.

No comments:

Post a Comment