Saturday, April 22, 2017

WAZIRI WA ELIMU: IRAN INAONGOZA DUNIANI KWA KASI YA MAENDELEO YA KIELIMU

Waziri wa Sayansi, Utafiti na Teknolojia wa Iran amesema, kwa mujibu wa takwimu mpya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inaongoza kwa kuwa na kasi kubwa zaidi ya maendeleo ya kielimu duniani.
Muhammad Farhadi ameyasema hayo leo pembeni ya ufunguzi wa shughuli za utendaji wa kituo cha makongamano ya kisayansi cha Chuo Kikuu cha Abu Ali Sinaa kilichoko mkoani Hamedan magharibi mwa Iran.
Amefafanua kuwa, katika mashindano na nchi 25 zenye ustawi wa kuendelea wa kielimu na kisayansi, Iran inongoza kwa kuwa na kasi ya ukuaji wa kielimu wa asilimia 14.
Waziri wa Sayansi, Utafiti na Teknolojia wa Iran ameongeza kuwa Russia na China ndizo zinazofuatia baada ya Iran katika orodha hiyo.
Amesema katika nyanja nyenginezo ikiwemo ya teknolojia pia, nafasi ya Iran imepanda kutoka 113 hadi 78 duniani; na kwa upande wa kieneo na Ulimwengu wa Kiislamu ndiyo inayoshika nafasi ya kwanza.
Mwanasayansi wa Kiirani akiwa katika utafiti
Awali akizungumza katika hafla hiyo, Naibu Waziri wa Sayansi, Utafiti na Teknolojia, anayehusika na masuala ya kimataifa Hussein Salar Aamoli alisema, kiwango cha ushirikiano wa kielimu baina ya vyuo vikuu vya Iran na vituo vya elimu duniani kimeongezeka.
Salar Aamoli aidha ameashiria utekelezwaji wa miradi tisa ya vyuo vikuu vya Iran kwa ushirikiano na vyuo vikuu vya juu duniani itakayogharimu zaidi ya yuro milioni moja  na kueleza kwamba idadi ya miradi ya pamoja ya kielimu baina ya Iran na wahadhiri wa vyuo vikuu vya nje katika mwaka uliopita ilifikia 235.../

No comments:

Post a Comment