Monday, April 24, 2017

UCHAGUZI WA RAIS WA IRAN KUFANYIKA KATIKA NCHI 102 DUNIANI

Tume ya Uchaguzi ya Iran imetangaza kuwa, uchaguzi wa rais wa awamu ya 12 wa Iran utafanyika katika nchi 102 kote duniani.
Katika taarifa, Katibu wa Tume ya Uchaguzi Ali Pur-Ali Mutlaq amesema Wairani wanaoishi nje ya nchi wataweza kupiga kura katika viituo 269 vya upigaji kura vilivyoko katika ofisi 131 za kidiplomasia za Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika nchi 102 kote duniani.
Ameongeza kuwa, wawakilishi wa Iran katika nchi hizo  tayari wameshapokea kila kitu kinachohusu uchaguzi wa rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran. Wagombea sita wa urais mwaka huu ni pamoja na Mostafa Aqa-Mirsalim ambaye ni waziri wa zamani wa utamaduni na muongozo wa Kiislamu, Mostafa Hashemi-Taba makamu wa rais wa zamani ambaye pia aliwahi mkuwa mkuu wa kamati ya kitaifa ya Olimpiki, Es'haq Jahangiri makamu wa kwanza wa serikali ya sasa, Mohammad-Baqer Qalibaf meya wa mji wa Tehran, Seyyed Ebrahim Raeisi msimamizi wa Haram Takatifu ya Imam Ridha AS na rais wa sasa  Hassan Rouhani ambaye anatetea nafasi yake ili amalize kipindi chake cha pili.
Zoezi la upigaji kura Iran
Uchaguzi wa 12 wa Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran unatarajiwa kufanyika Ijumaa ya tarehe 19 mwezi ujao wa Mei sambamba na uchaguzi wa tano wa mabaraza ya Kiislamu ya miji na vijiji kote nchini Iran. Wairani wanaoishi nje ya nchi wanaweza kushiriki katika uchaguzi wa rais pekee.

No comments:

Post a Comment