Monday, April 17, 2017

MAKUMI YA ASKARI WA SAUDIA WAANGAMIZWA NA WALENGA SHABAHA WA YEMEN

Jeshi la Yemen limetangaza kuwa, walenga shabaha miongoni mwa jeshi la nchi hiyo na harakati ya Answarullah wamefanikiwa kuwaangamiza makumi ya askari wa Saudia katika mkoa wa Ma'rib, katikati mwa nchi hiyo.
Kikosi cha walenga shabaha katika jeshi la Yemen na harakati ya Answarullah kimetangaza kuwa, askari hao wa Saudia wameangamizwa katika operesheni iliyojiri katika eneo la al-Rabia, al Zughan, al Mashjah, al far'u, Kufal na al-Mukhadarah. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, askari wengine 11 wa Saudia wameangamizwa pia katika operesheni ya barabarani baada ya kutega bomu lililolipuliwa na jeshi la Yemen na kuwaangamiza askari hao vamizi karibu na kambi ya jeshi ya Habs, mkoa wa Jizan.
Askari vibaraka wanaoshiriki katika hujuma za Saudia Yemen baada ya kuuawa
Aidha askari mwingine wa gadi ya ulinzi wa mpakani na polisi watatu wote wa Saudia wameangamizwa kwa kupigwa risasi katika eneo la mpakani la Jizani baina ya nchi hiyo na Saudia. Katika hatua nyingine jeshi la Yemen na harakati ya wananchi limeshambulia eneo walipokusanyika askari vibaraka wa Saudia katika mji wa al-Mokha, mkoa wa Taiz na kuwasababishia hasara kubwa. Hii ni katika hali ambayo ndege za kivita za Saudia zimeshambulia maeneo ya raia ya Maqbanah, mkoa wa Taiz na kusababisha raia kadhaa kuuawa na wengine wengi kujeruhiwa.

No comments:

Post a Comment