Thursday, June 8, 2017

MAWAHABI WADHANIWA KUFANYA MASHAMBILIZI YA KIGAIDI MJINI TEHRANI, IRAN

Wizara ya Usalama wa Taifa ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imesema kuwa, magaidi waliofanya mashambulizi jana Jumatano hapa Tehran wametambuliwa. Imesema, magaidi hao walikuwa na uhusiano wa moja kwa moja na magenge ya Kiwahabi nje ya Iran.
Wizara ya Usalama wa Taifa ya Iran imesema hayo leo katika taarifa yake maalumu na kuongeza kuwa, timu ya magaidi hao wa Daesh (ISIS) ambao jana walishambulia Haram ya Imam Khomeini MA na eneo la Bunge la Iran walikuwa ni magaidi watano ambao wana historia ya vitendo vya uhalifu na walikuwa wanachama wa magenge ya Kiwahabi ya wakufurishaji.
Taarifa hiyo imeongeza kuwa, baada ya kujiunga na genge la kigaidi la Daesh, magaidi hao walishiriki kwenye jinai za genge hilo huko Mosul, kaskazini mwa Iraq na Raqqah, kaskazini mwa Syria. 
Operesheni ya kupambana na magaidi wa Daesh katika majengo ya Bunge mjini Tehran, Jumatano, Juni 8, 2017

Taarifa ya Wizara ya Usalama wa Taifa ya Iran imeongeza kuwa, katika msimu wa joto wa mwaka jana, magaidi hao waliingia nchini Iran wakiongozwa na Abu Ayesheh, mmoja wa makamanda wa ngazi za juu wa magaidi wa Daesh kwa lengo la kufanya mashambulio kadhaa ya kigaidi katika miji ya kidini ya Iran. Hata hivyo maafisa usalama wa Iran walisambaratisha kikamilifu kundi hilo ikiwa ni pamoja na kumwangamiza Abu Ayesheh. Baadhi ya magaidi wa timu hiyo walifanikiwa kutoroka wakiwemo magaidi hao watano waliofanya mashambulizi ya kigaidi jana Jumatano hapa mjini Tehran.
Magaidi hao walioangamizwa jana mjini Tehran wametambuliwa kwa majina ya: Seriyas, Fereydoun, Qayyoum, Abu Jahad na Ramin. Jana Jumatano tarehe 8 Juni 2017, mji wa Tehran ulishuhudia mashambulizi mawili ya kigaidi katika Haram ya Imam Khomeini (quddisa sirruh) na jengo la kiidara la Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran). 

No comments:

Post a Comment