Friday, July 28, 2017

MAREKANI YARUSHA KOMBORA KUIJIBU KOREA KASKAZINI

Korea Kusini na Marekani wamefanya zoezi la pamoja la kurusha makombora ya ardhini baada ya Korea Kaskazini kufanya jaribio jingine la kombora. Afisa wa Ulinzi wa Marekani alithibitisha kufanyika kwa zoezi hilo la kulipiza kisasi bila ya kutoa taarifa zaidi. Korea Kaskazini ilirusha kombora la masafa marefu linaloweza kuruka kutoka bara moja hadi jingine hapo jana, ambalo wataalamu wanasema lina uwezo wa kufikia miji kadhaa ya Marekani. Wizara ya Ulinzi ya Marekani Pentagon imesema kombora hilo la Korea Kusini liliruka umbali wa kilomita 1,000 kabla ya kuanguka katika Bahari ya Japan. Rais wa Marekani Donald Trump amelilaani jaribio hilo la pili la Korea Kaskazini la kombora la kuruka kutoka bara moja hadi jingine na kulitaja kuwa ni kitisho kwa ulimwengu.

No comments:

Post a Comment