Tuesday, June 12, 2018

MAGAZETI YA UJERUMANI YAMKOSOA TRUMP, YAMWITA "MPUMBAVU"

Magazeti ya Ujerumani yamemtaja Rais Donald Trump wa Marekani kuwa ni mtu asiyejua mipaka yake wala asiye na mantiki na yamezitaka nchi zote za Ulaya kuacha kumfuata kiongozi huyo.
Gazeti la Ujerumani la Süddeutsche Zeitung limeripoti kuwa, kila mtu aliyekuwa anaamini kuwa Rais wa Marekani ni mtu mwenye mantiki na anayetilia maanani uhakika wa mambo anapaswa kuzika matumaini hayo kwa sababu kuwepo kwa mtu huyo asiye na adabu na mbumbavu hakuifanyi dunia kuwa sehemu bora na yenye amani zaidi.
Gazeti hilo la Ujerumani limeongeza kuwa: Trump anaendelea kuzitishia nchi nyingine kwa kutumia mabavu na silaha ya uchumi, na suala hilo ni hatari sana kwa Ujerumani.
Trump na Macron
Süddeutsche Zeitung limeandika kuwa: Nchi za Magharibi zimekumbwa na mgawanyiko katika masuala ya kisiasa na uhakika huo umeonekana waziwazi katika mkutano wa viongozi wa nchi 7 zilizopiga hatua kiviwanda wa G7 huko Canada ambao kimsingi ulibadilika na kuwa G6. 
Rais Donald Trump wa Marekani siku chache zilizopita aliwaacha bumbuazi viongozi wengine wa G7 katika mkutano wa Canada baada ya kuondoka ghafla katika mkutano huo na kufuta saini yake katika hati ya mwisho ya mkutano huo. 

No comments:

Post a Comment