Sunday, May 27, 2018

WATU 30 WAUAWA KATIKA MAPIGANO MASHARIKI MWA KONGO DR

Watu 30 wameuawa katika mapigano kati ya jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na wanamgambo wa Mai-Mai mashariki mwa nchi hiyo.
Duru za eneo hilo zimeripoti kuwa katika mapigano hayo yaliyotokea jana na kuendelea kwa saa kadhaa wanajeshi 18 waliuawa akiwemo afisa mmoja na kamanda wa polisi wa polisi wa eneo hilo.
Kwa mujibu wa duru hizo, wanamgambo wanane waliohusika katika hujuma hiyo pamoja na raia watatu pia waliuawa katika mapigano hayo. Raia hao waliuliwa kwa risasi walipokuwa wakikimbia mapigano.


Mnamo siku ya Alkhamisi iliyopita, wanamgambo wa kundi la Mai-Mai walilidhibiti eneo lenye utajiri wa madini la Salamambila mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, lakini wakalazimika kuliacha na kukimbia baada ya vikosi vya jeshi la serikali kufika katika eneo hilo.
Wanamgambo wa Mai-Mai wanatokana na makundi ya wabeba silaha waliopata mafunzo ya kijeshi katika eneo la mashariki mwa Kongo DR ambalo limekuwa uwanja wa mapigano kwa zaidi ya miaka 20 sasa.../

No comments:

Post a Comment