Saturday, May 19, 2018

RAIS RTUMP WA MAREKANI AWATUSI TENA WAHIJIRI KWA KUWAITA KUWA NI WANYAMA

Rais Donald Trump wa Marekani kwa mara nyingine ametoa matamshi mabaya yenye kuwavunjia heshima wahajiri au wahamiaji nchini humo kwa kuwataja kuwa ni wanyama.
Matamshi hayo ya Trump si ya kwanza ya aina yake kwani miezi kadhaa iliyopita katika kikao chake na wajumbe wa vyama vya Democrat na Republican katika Ikulu ya White House aliashiria kuhusu wahajiri kutoka Haiti, El Salvador na baadhi ya nchi za Afrika na kuzitaja kuwa sawa na shimo la kinyesi.
Matamshi hayo ya mara kwa mara ya Trump ya kuwavunjia heshima wahamiaji hasa wenye asili ya Afrika yamekosolewa na wajumbe wa chama cha upinzani cha Democrat ambao wanasema ni ishara ya wazi kuwa mtawala huyo ni mbaguzi wa rangi.
Ikulu ya White House ilijaribiu kuonyuesha kuwa matamshi hayo yalitokana na hisia za kitaifa za rais huyo, lakini baada ya kuendelea malalamikio kuhusu matamshi hayo ya kishenzi ya Trump, rais huyo akiwa katika mkutano na Katibu Mkuu wa Shirika la Kijeshi la Nato, katika kujaribu kutetea matusi yake kuhusu wahajiri wanaoingia nchini humo kinyume cha sheria, amesema wakati alipowahutubu kwa kuwaita kuwa ni 'Wanyama' siku ya Jumatano, alikusudia genge la wahalifu linalojulikana kama  'MS 13'.
Matamshi hayo ya Trump kuhusu wahajiri ambayo aliyatoa wakati wa mkutano wake na wakuu wa jimbo la California, yamekosolewa vikali na wajumbe wa Bunge la Kongresi.
Mtu mwenye asili ya Afrika akikandamizwa nchini Marekani
Aghalabu ya wajumbe wa Kongresi wanaamini kuwa matamshi hayo yasiyokubalika hata kidogo ya Trump, yanaonyesha wazi kuwa hawajibiki na ni mchochezi.
Matamshi hayo ya Trump ya kuwavunjia heshima na kuwadhalilisha wahajiri yameandamana na hatua za kivitendo za kuwatenganisha watoto wahajiri na wazazi wao.
Hali kadhalika Trump amewawekea Waislamu vizingiti kuingia Marekani sambamba na hatua zingine nyingi za kibaguzi. Hatua hizo za Trump zinalenga kuwashinikiza wahajiri na wahamiaji ili kuwazuia wasiingie Marekani.
Matamshi ya kibaguzi ya rais wa Marekani ni chanzo cha wasiwasi na hofu katika jamii ya Marekani hasa miongoni mwa wasomi nchini humo ambao wanaamini kuwa matamshi hayo yasiyofaa hata kidogo yataharibu itibari iliyobakia ya nchi hiyo duniani.
Rupert Colville, Msemaji wa Ofisi ya Haki za Binadamu katika Umoja wa Mataifa anasema matamshi ya Trump ni ya kushtua na ya kuaibisha.
Ikulu ya White House na hata Donald Trump mwenyewe wamejaribu kukanusha matamshi hayo ya kibaguzi, lakini ukweli usioweza kupingika ni huu kuwa, ubaguzi wa rangi ni sehemu ya utambulisho wa wazi wa utawala wa Rais Trump na Ikulu ya White House.

No comments:

Post a Comment