Sunday, May 27, 2018

BAYTU ZAKAT YA KUWAIT YAZINDUA PROGRAMU YA DOLA 26400 KWA AJILI YA KUFUTURISHA KATIKA MWEZI WA RAMADHAN NCHINI TANZANIA


 Balozi wa Kuwait nchini Tanzania Mhe. Jasem Al-Najem anashiriki katika utekelezaji wa programu ya kufuturisha ndani ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhan ambayo inafadhiliwa na Chombo cha Baytu Zakat, Wakfu na Mali ya Amana ya Kuwait. Programu kama hii huandaliwa kila mwaka kutoka kwa wasamaria wa nchi ya Kuwait.  
Programu hii thamani yake ni dola elfu 26 na mia nne sawa na shilingi milioni 60.
Awamu ya kwanza ya programu hii ilikuwa ni kugawa vikapu 400 vyenye vyakula kama mchele, sukari,unga,mafuta ya kula, tende na sukari ambapo katika moja ya zoezi la ugawaji alihudhuria Mkuu wa Wilaya ya Ilala. Bi Sophia Mjema.
Ubalozi wa Kuwait umedhamiria mwaka huu kuwasilisha misaada ya futari katika miji, vitongoji, kata, mitaa, vijiji na maeneo ya mbali kote Tanzania ambapo hadi sasa mikoa ya Tanga, Iringa, Dar es salaam na visiwa vya Zanzibar imefaidika na misaada hiyo ambayo Ubalozi hushirikiana na asasi zisizokuwa za kiserikali za Tanzania katika kuwafikia walengwa.







No comments:

Post a Comment