Tuesday, September 12, 2017

MASHIRIKA YA KUTETEA HAKI ZA BINADAMU YAIKOSOA UN KWA KUTOCHUKUA HATUA DHIDI YA MAUAJI YA WAISLAMU, MYANMAR

Jumuiya na mashirika ya kutetea haki za binadamu yamelikosoa vikali Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kutokana na kutochukua msimamo imara mbele ya jinai zinazoendelea kufanywa na jeshi na Mabudha wa Myanmar dhidi ya Waislamu wa jamii ya Rohingya nchini humo.
Mashirika hayo yanasema kinachofanyika nchini Myanmar ni maangamizi ya kizazi cha Waislamu wa Rohingya.
Mashirika hayo yameashiria jinai ya kuwalazimisha Waislamu zaidi ya laki tatu wa Myanmar kuyahama makazi yao katika kipindi cha kuanzia tarehe 25 mwezi uliopita na kusisitiza udharura wa kusitishwa uhalifu kama huo. Mashirika hayo pia yamezitaka nchi wanachama wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa zinazotazamiwa kukutana leo mjini New York kwa ajili ya kuchunguza mgogoro wa Myanmar, zichukua hatua za maana katika uwanja huo. 
Waislamu wa Myanmar wakilazimishwa kuhama makazi na vijiji vyao
Siku chache zilizopita pia Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Iran, Muhammad Javad Zarif alimwandikia barua Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa akiitaka jamii ya kimataifa kuchukua hatua za kusitisha ukatili unaofanyika kwa mpangilio maalumu dhidi ya Waislamu nchini Myanmar.
Tangu Ijumaa ya tarehe 25 Agosti Waislamu wasiopungua elfu 6 na 334 wa jamii ya Rohingya nchini Myanmar wameuwa na wengine zaidi ya elfu 8 kujeruhiwa katika wimbi jipya la mashambulizi na ukandamizaji unaofanywa na jeshi la nchi hiyo dhidi ya Waislamu katika mkoa wa Rakhine.

Monday, September 4, 2017

KIONGOZI WA CIA AMUONYA TRUMP KUTOKANA NA MATAMSHI YAKE MAKALI DHIDI YA KOREA KASKAZINI

Mkuu wa zamani wa Shirika la Kijasusi la Marekani CIA, Michael Hayden amemuonya Rais Donald Trump wa Marekani kutokana na kutoa matamshi makali dhidi ya Korea Kaskazini.
Michael Hayden ameyasema hayo leo Jumatatu na kuongeza kuwa, matamshi ya rais huyo wa Marekani dhidi ya Pyongyang, yanaweza kuzusha maafa makubwa. Kiongozi huyo zamani wa Shirika la Kijasusi la Marekani CIA ameongeza kuwa, baadhi ya matamshi yaliyotolewa na Trump si ya mantiki. Kabla ya hapo Rais Donald Trump alitoa matamshi makali dhidi ya Korea Kaskazini akitishia kuishambulia kijeshi nchi hiyo ya Asia.
Michael Hayden, Mkuu wa zamani wa Shirika la Kijasusi la Marekani CIA
Matamshi na misimamo ya rais huyo wa Marekani imepelekea kuongezeka mgogoro katika eneo la Peninsula ya Korea. Kufuatia miamala hiyo ya Trump, serikali ya Pyongyang nayo imeendelea kujiimarisha kijeshi kukabiliana na chokochoko za Washington na washirika wake katika eneo hilo. Wakati huo huo, serikali ya China imeionya Korea Kaskazini juu ya hatua yake ya kuendelea kuyafanyia majaribio makombora yake ya balestiki. Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China,  Geng Shuang amesema kuwa, Pyongyang haitakiwi kuifanya hali ya mambo katika eneo la Korea kuzidi kuwa mbaya zaidi na kwamba viongozi wa Korea Kaskazini ni lazima wafahamu kuwa, maazimio ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa yamekataza mwenendo huo.
Geng Shuang , Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China
Kadhalika Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Uchina amesisitiza kuwa, Beijing inatumai kwamba pande zote za mgogoro zitajizuia kutokana na hatua zinazoweza kuchochea zaidi mvutano katika eneo la Peninsula ya Korea.KIO

JESHI LA IRAN: TUTAEDELEZA KUZISAIDIA NCHI JIRANI KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA UGAIDI

Mkuu wa Vikosi vya Ulinzi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Jenerali Muhammad Hossein Baqeri amesema kuwa Iran itaendelea kuzisaidia nchi majirani katika vita dhidi ya makundi ya kigaidi.
Jenerali Hossein Baqeri ameyasema hayo leo katika maonyesho ya 'Mafunzo ya Umahiri" ya askari yaliyofanyika hapa mjini Tehran na kuongeza kuwa, licha ya kuwepo njama mbalimbali za adui na ukwamishaji mambo wa mabeberu wa dunia, lakini Vikosi vya Ulinzi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran chini ya Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu na uungaji mkono wa wananchi, imeendelea kupata mafanikio makubwa katika operesheni zake za kulinda usalama.
Mkuu wa Vikosi vya Ulinzi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Jenerali Muhammad Hossein Baqeri 
Aidha amesema kuwa, Iran ya Kiislamu imeendelea kutoa msaada kwa nchi majirani katika kukabiliana na ugaidi. Jenerali Hossein Baqeri amezungumzia maonyesho hayo na kusema kuwa mafunzo hayo ya umahiriyna lengo la kuwaweka tayari askari wa vikosi vya ulinzi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa ajili ya vita yoyote wakati adui atakapoanzisha mashambulizi yake dhidi ya Iran. Maonyesho hayo yamehudhuriwa na makamanda wa ngazi ya juu na viongozi mbalimbali wa serikali ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran hapa mjini Tehran.

Friday, September 1, 2017

MAREKANI YAPIGA MARUFUKU RAIA WAKE KWENDA KORA KASKAZINI

Wizara ya mambo ya kigeni ya Marekani imepiga marufuku raia wake kwenda Korea kaskazini hatua ambayo inaanza rasmi leo Ijumaa (01.09.2017),wakati nchi hizo zikilumbana kuhusu dhamira ya Pyongyang kujitengezea silaha.

Nordkorea - US-Student Otto Warmbier (picture alliance/dpa/MAXPPP)
Otto Warmbier alipokamatwa na polisi wa Korea kaskazini
Wakati  huo  huo waziri  wa mambo  ya  kigeni  wa  Ufaransa amesema  Korea  kaskazini ina uwezo wa  kurusha makombora ya  masafa marefu  katika  miezi michache  ijayo na  kuitaka  China  kuchukua  hatua  zaidi  kutatua mzozo  huo.
Hatua  ya  kupiga  marufuku  raia  wa  marekani  kutembelea  Korea kaskazini  imechukuliwa  kutokana  na  kifo  cha  mwanafunzi  Otto Warmbier  mwezi  Juni, siku  chache  baada  ya  kijana  huyo mwenye  umri  wa  miaka  22  kurejeshwa  nyumbani   akiwa hajitambua  kufuatia  kufungwa  jela  kwa  zaidi  ya  mwezi  mmoka nchini  humo.
Nordkorea Kim Jong-Un (Reuters/KCNA)
Kiongozi wa Korea kaskazini Kim Jong Un
Alihukumiwa  kwa  kosa  la  kula  njama  dhidi  ya  taifa  hilo  kwa kujaribu  kuiba  bango  la  propaganda  kutoka  katika  hoteli  mjini Pyongyang  na   kuhukumiwa  kifungo  cha  miaka  15  na  kazi ngumu, huku  rais  Donald Trump  akiulaumu  utawala  wa  kinyama wa  Pyonyang , kwa  hali  madhara  aliyoyapata.
Katika  tovuti  yake , wizara  ya  mambo  ya  kigeni  ya  Marekani imesema  imechukua   uamuzi  huo  kutokana  na "hali  mbaya  na kitisho  kinachoongezeka  cha  kukamatwa  na  kufungwa  kwa kipindi  kirefu raia  wa  Marekani".
Wamarekani  watatu  wanaoshutumiwa  kwa  uhalifu mbali  mbali dhidi  ya  taifa  hilo  wako jela  nchini  Korea  kaskazini, nchi  ambayo imo  katika  hali  ya  mvutano  na  wasi  wasi  mkubwa   na  utawala wa  Trump  kuhusiana  na  mpango  wake  uliopigwa  marufuku  wa silaha  za  kinyuklia.
Mapema  wiki  hii  Pyongyang  ilifyatua  kombora  kupitia  anga  ya Japan , katika  hatua  ya  juu  kabisa  ya  kuchochea  mzozo  huo, na imetishia  kurusha  makombora  zaidi  kuelekea  kisiwa  cha  Guam ambacho  kinamilikiwa  na  Marekani  katika  bahari  ya  Pasifiki.
Majaribio  ya  Korea  kaskazini
Mwezi  Julai  Korea  kaskazini  ilifanya  majaribio  yake  mawili yaliyofanikiwa   ya  makombora  ambayo  yana uwezo  wa  kuruka kutoka  bara  moja  kwenda  lingine, na  hatimaye  kuweza  kufika nchini  Marekani.
Nordkorea Raketenstart (Reuters/KCNA)
Kombora la Korea kaskazini
Marufuku  hiyo  hata  hivyo  haiwagusi waandishi  habari, wawakilishi wa  shirika  la  msalaba  mwekundu, wale  wanaosafiri  kwa madhumuni  ya  kutoa  msaada  wa  kiutu , ama  safari  ambazo wizara  ya  mambo  ya  kigeni  inaziona  kuwa  na  maslahi  na Marekani. Lakini  asasi  za  kijamii  zinazofanyakazi  nchini  Korea kaskazini kibinafsi  zimeeleza  wasi  wasi  wake  juu  ya  vipi  hatua hiyo  itafanyakazi  na  athari  zake  katika  kazi  yao. 
Raia wachache  wa  Marekani  ambao  wamebaki  nchini  humo wameondoka  siku  ya  Alhamis, zimesema  baadhi  ya  ripoti. Waziri anayehusika  na  kuziunganisha  Korea mbili  wa  Korea  kusini  Lee Eugene amesema  Korea  kaskazini  inapaswa  kuacha  uchokozi.
"Korea  kaskazini  inaendelea  kufanya uchokozi. Msimamo  wa serikali  yetu  kwamba  tunahitaji  suluhisho  la  amani katika  suala la  kinyuklia  la  Korea  kaskazini  na rasi  ya  Korea haujabadilika. Pia , tunaitaka  Korea kaskazini  kuacha kutoa  matamshi  ya ukosoaji  na  vitisho  na  kuchukua  njia  ya  mazungumzo na ushirikiano."
Zentralafrika Bangui - Französischer Verteidigungsminister Jean-Yves Le Drian bei Militärbasis (Reuters/Stringer)
Waziri wa mambo ya kigeni wa Ufaransa Jean-Yves Le Drian
Wakati  huo  huo waziri  wa  mambo  ya  kigeni  wa  Ufaransa  Jean-Yves Le Drian  amekiambia  kituo  cha  redio  cha  RTL  kwamba hali  ni  mbaya , tunaona  Korea  kaskazini  ikiwekea  malengo  ya kesho  ama  kesho  kutwa  kurusha  makombora  yenye  vichwa  vya kinyuklia. Kwa  wakati  huu  ambapo  Korea  ya  kaskazini  ina uwezo  wa  kushambulia  Marekani , hata  Ulaya, lakini  hasa  Japan na  China, hali  itakuwa  mbaya  zaidi.
Le Drian  ambae  alizungumza  na  mwenzake  wa  China  siku  ya Alhamis , amesema  kila  kitu kinapaswa  kufanywa  kuhakikisha vikwazo  vya  hivi  karibuni  vya  umoja  wa  Mataifa  vinatekelezwa na  kuitaka  China , mshiriam mkubwa  wa  kibiashara  wa Pyonyang, kuchukua  juhudi  zote  kuvitekeleza.

MAHAKAMA YA JUU KENYA YAAMURU UCHAGUZI MPYA WA RAIS

Mahakama ya Juu nchini Kenya imeamuru kurejewa kwa uchaguzi wa rais nchini humo, ikiyafuta yale ya awali yaliyokuwa yamempa ushindi Rais Uhuru Kenyatta. 
Kenias Oberstes Gericht (picture-alliance/AP Photo/S. Azim)
Mahakama hiyo imesema kulikuwa na ukiukwaji mkubwa wa taratibu kwenye uchaguzi wa tarehe 8 Agosti kiasi cha kuvunja hata katiba ya taifa hilo la Afrika Mashariki. 
Uchaguzi mpya umeamuriwa kufanyika ndani ya siku 60 kutoka sasa. 
Mgombea wa upinzani, Raila Odinga, alikuwa amedai kuwa matokeo ya kura kwa njia ya elektroniki yalidukuliwa na kuchakachuliwa kumsaidia Uhuru Kenyatta wa chama tawala, Jubilee. 
Tume ya Uchaguzi na Mipaka, IEBC, ilikuwa imemtangaza Kenyatta mshindi wa asilimia 54 ya kura.
Wakeya kadhaa waliamua kuingia mitaani kupinga matoeo hayo na walikuwa wamedhamiria kuingia tena endapo mahakama ingelipitisha ushindi huu. 
Hii ni mara ya pili kwa Odinga kupinga matokeo mahakamani, lakini mwaka 2013 alishindwa.

TUME YA UCHAGUZI DRC KUTANGAZA RATIBA YA UCHAGUZI

Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Corneille Nangaa amesema ratiba ya Uchaguzi mkuu itatangazwa hivi karibuni.
Kauli hiyo imekuja siku moja baada ya tume hiyo kutangaza kuwa jumla ya wapiga kura milioni 40 wameandikishwa kwenye majimbo 24 na kwamba kuanzia tarehe nne itaanza kuandikisha wapiga kura kwenye majimbo mawili ya Kasai.
Serikali ya Kinshasa imesema zoezi la kuandikisha wapiga kura litaanza kukamilika kabla ya kutangazwa mambo mengine.
Mapema wiki hii Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya DRC (CENI) ilisema, zoezi la kuhakiki na kuandikisha wapiga kura wapya kwenye majimbo mawili ya Kasai ambako kumeshuhudiwa machafuko hivi karibuni, litaanza September 4 na kisha kuendelea kwenye majimbo mengine 24
Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi CENI, Corneille Nangaa amewataka wananchi kuwasaidia maofisa wake kufanya kazi ya kuandaa uchaguzi kwa uhuru.
Rais Joseph Kabila
Katika hatua nyingine upinzani umekosoa takwimu za hivi karibuni zilitolewa na tume hiyo ukisema kwamba kiwango kikubwa hakiko sawa.
CENI ilisema jumla ya wapiga kura milioni 40 wameandikishwa kwenye majimbo mengine 24 huku taifa hilo likiwa na jumla ya raia milioni 70 wengi wao wakiwa bado hawajaandikishwa.
Mgogoro wa ndani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo uliibuka baada ya kuahirishwa tarehe ya uchaguzi wa rais na kadhalika sisitizo la Rais Joseph Kabila la kutaka kuendelea kubakia madarakani. Licha ya kutiwa saini makubaliano baina ya wapinzani na serikali juu ya kufanyika uchaguzi wa rais tarehe 31 mwezi Disemba mwaka huu, lakini inaonekana kuwa, uchaguzi huo hautaweza kufanyika katika tarehe iliyopangwa.

WAISLAMU 400 WAFARIKI DUNIA MYANMAR KATIKA KIPINDI CHA WIKI MOJA

  • Waislamu 400 wafariki dunia Myanmar katika kipindi cha wiki moja
Waislamu takribani 400 wamefariki dunia nchini Myanmar katika kipindi cha wiki moja tokea jeshi la nchi hiyo lianzishe kampeni mpya ya kuwakandamiza Waisalmu wa jamii ya Rohingya.
Takwimu ramsi zinaonyesha kuwa watu 400 wamepoteza maisha katika jimbo la Rakhine tokea Ijumaa iliyopita. Kati ya walipooteza maisha ni wale waliouliwa na jeshi la nchi hiyo katika oparesheni  dhidi ya Waislamu huku wengine, wakiwemo wanawake na watoto wadogo, wakipoteza maisha wakati wakivuka mto kukimbia mapigano katika jimbo la Rakhine.
Jeshi la Myanmar Ijumaa iliyopita lilianzisha oparesheni kali dhidi ya Waislamu kwa madai kuwa watu wanaodaiwa kuwa ni Waislamu walihujumu vituo vya polisi jimboni Rakhine.
Mabuddha wenye misimamo mikali
Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa, Waislamu wa kabila la Rohingya ni jamii ya wachache inayodhulumiwa na kunyongeshwa zaidi duniani. 
Katika miaka ya karibuni, Waislamu wengi wa kabila la Rohingya nchini Myamnar wameuawa au kulazimika kuhama makazi yao na kuwa wakimbizi katika nchi za Bangladesh, Thailand, Malaysia na Indonesia kutokana na mashambulio ya Mabudha wenye misimamo ya kufurutu mpaka wanaoungwa mkono na serikali ya nchi hiyo.