Sunday, March 26, 2017

HRW YATAKA RAIS WA SUDSN SZUIWE KUINGIS JORDDN AU AKAMATWE

Shirika la kimataifa la Haki za Binadamu HRW limetaka Rais Omar al Bashir wa Sudan azuiwe kuingia nchini Jordan.
Kwa mujibu wa shirika la habari la AFP, Human Rights Watch imetoa tamko la kuitaka serikali ya Jordan imma imzuie Rais Omar al Bashir kutembele nchi hiyo au imtie mbaroni mara atakapowasili nchini humo.
Taasisi hiyo ya kimataifa isiyo ya kiserikali imegusia tuhuma zinazomkabili Rais wa Sudan za kuhusika katika jinai za kivita za jimbo la Darfur la magharibi mwa nchi hiyo na kuitaka serikali ya Jordan iheshimu makubaliano ya kimataifa.
Katika tamko lake hilo Human Rights Watch imesema, kwa vile Jordan ni mwanachama wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC, ina wajibu wa kutekeleza makubaliano yaliyounda mahakama hiyo. Shirika hilo la haki za binadamu limedai pia kuwa, kama Jordan itamruhusu Rais al Bashir kutembelea nchi hiyo au kama haitomtia mbaroni, itakuwa imekwenda kinyume na ahadi zake kwa mujibu wa makubaliano ya ICC. 
Mahakama ya ICC inadai kuwa Rais Omar al Bashir wa Sudan amehusika katika jinai za kivita katika jimbo la Darfur na imetoa waranti wa kutiwa mbaroni.
Kikao cha wakuu wa Jumuia ya Nchi za Kiarabu kimepangwa kufanyika Jumatano ya tarehe 29 mwezi huu wa Machi nchini Jordan. Rais Omar al Bashir amealikwa kushiriki kwenye kikao hicho.
Jimbo la Darfur la magharibi mwa Sudan lilikumbwa na machafuko tangu mwaka 2003 kulalamikia kudharauliwa na kutelekezwa na serikali.

IRAN YATAKA MAREKANI ISHTAKIWE KWA JINAI ZA KIVITA BAADA YA MAUAJI YA MOSUL

Afisa wa ngazi za juu nchini Iran amesema kuwa, hujuma za ndege za kivita za Marekani katika mji wa Mosul, Iraq ambazo zimeua idadi kubwa ya raia, ni jinai za kivita.
Ali Shamkhani, Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran amesema, jinai iliyofanywa na Marekani huko Mosul ni sawa na jinai za kivita zinazofanywa na magaidi wa Daesh (ISIS) pamoja na makundi mengine ya magaidi wakufurishaji ambao wanawalenga raia na watu wasio na hatia. Amesema jinai hizo za Marekani zinapaswa kushughulikiwa haraka iwezekanavyo katika mahakama ya kimataifa.
Siku ya Jumamosi Marekani ilikiri ilifanya mashambulizi ya angani huko magharibi mwa Mosul mnamo Machi 17 mwaka huu na kuua raia 200. Wakuu wa Iraq wanasema Mareknai ilifanya hujuma kadhaa siku hiyo.
Maeneo ya raia yaliyohujumiwa na Marekani huko Mosul, Iraq
Shamkhani amesema, hata kama Marekani inadai eti hujuma hiyo haikuwa ya makusudi, lakini hilo haliwaondoi hatiani Wamarekani waliotenda jinai hiyo. Shamkhani amesema, jeshi la Marekani limekuwa likiua raia wasio na hatia katika eneo hili kwa kisingizo cha kupambana na ugaidi.
Umoja wa Mataifa pia umetangaza kushtushwa na kupoteza maisha raia katika shambulio hilo la Marekani mjini Mosul, kaskazini mwa Iraq.

IGAD; WAKIMBIZI WAHIFADHIWE KWA MUJIBU WA SHERIA ZA KIMATAIFA

mediaWaziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam DesalegnPhoto: Reuters/Tiksa Negeri
Mkutano wa IGAD umefunguliwa rasmi jumamosi jijini Narobi ambapo wito umetolewa na viongozi wa nchi wanachama wa shirika hilo kufanya kila wawezalo kuhakikisha kuwa wakimbizi wanapewa hifadhi bila kujali nchi wanazotoka.
Waziri mkuu wa Ethiopia, Hailemariam Dusalegn alisisitiza wanachama kuwa wakimbizi lazima wahifadhiwe kwa vyovyote vile Kulingana na sheria za kulinda wakimbizi za kimataifa.
Hadi sasa raia wa Somalia wapatao Milioni mbili wameyakimbia makwao huku wengi wakiishi nchini Kenya, Ethiopia na nchini Uganda.
Umoja wa Mataifa umekuwa ukitoa wito kwa nchi za hasa Kenya kuendelea kuwapa hifadhi wakimbizi wa Somalia.

WANAJESHI KADHAA WA MISRI WAUAWA KATIKA MRIPUKO WA BOMU SINAI

Wanajeshi wanne wa Misri wameuawa baada ya gari lao kulengwa kwa bomu katika Peninsula ya Sinai.
Duru za kijeshi zimearifu kuwa, mlipuko huo ulitokea yapata kilomita 20, kusini mwa mji wa al-Arish, kaskazini mwa eneo la Sinai.
Habari zaidi zinasema kuwa, watu kadhaa wamejeruhiwa katika shambulizi hilo la bomu, linaloaminika kufanywa na magenge ya kigaidi yanayofungamana na kundi la kitakfiri la Daesh.
Vikosi vya Misri eneo la Sinai
Shambulizi hilo la jana limefanyika siku mbili baada ya hujuma nyingine kama hiyo ya bomu kuua askari 10 wa jeshi la Misri katikati mwa Peninsula ya Sinai. Hata hivyo, vyombo vya usalama vya nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika vilifanikiwa kuangamiza magaidi 15 katika operesheni hiyo, mbali ya kuwatia mbaroni wengine 7. 
Eneo la Sinai Kaskazini limekuwa likishuhudia mashambulizi ya mara kwa mara ya kundi la Ansar Baytul Muqaddas, tawi la genge la kigaidi la Daesh nchini Misri, hujuma zilizoshadidi baada ya kundi hilo kutangaza utiifu kwa kundi la kigaidi la Daesh mwaka 2014.

MAANDAMANO SANA'A KULAANI VITA VYA SAUDIA DHIDI YA YEMEN

Mamilioni ya wananchi wa Yemen wameandamana leo katika mji mkuu Sana'a na maeneo mengine nchini humo katika mwanzo wa mwaka wa tatu tokea Saudia ianzishe vita vyake vya kinyama dhidi ya nchi hiyo ambavyo vimesababisha maelfu ya watu kupoteza maisha na wengine wengi kupoteza makazi yao.
Katika maandamano hayo yaliyofanyika leo Jumapili katika Medani ya Al Sabin mjini Sana'a, Wayemen walikuwa wamebeba bendera za nchi yao huku wakitoa nara dhidi ya umwagaji damu unaofanywa na Saudia nchini humo kwa muda wa miaka miwili.
Akizungumza katika maandamano hayo, Saleh al Samad, Rais wa Baraza Kuu la Kisiasa la Yemen amewapongeza Wayemen kwa kusimama kidete kupambana na wavamizi wa Aal Saud. Amesema Saudi Arabia imeshindwa kufikia malengo yake nchini Yemen pamoja na kuwa imetumia kiasi kikubwa cha fedha na silaha za kisasa.
Lengo kuu la mashambuliai ya Saudia dhidi ya Yemen ni kumrejesha madarakani kibaraka wake, Rais wa zamani wa nchi hiyio aliyejiuzulu na kutoroka nchi Abdu Rabuh Mansour Hadi. Lengo jingine ni kutaka kuwaondoa madarakani wanamapinduzi wa Ansarullah.
Uharibifu wa Saudia katika makazi ya raia nchini Yemen
Tangu ulipoanzisha uvamizi wake wa kijeshi dhidi ya Yemen mwezi Machi mwaka 2015 hadi sasa, muungano vamizi wa kijeshi unaoongozwa na utawala wa Aal Saud na kuungwa mkono na Marekani na Israel umeshaua zaidi ya watu 12,000 katika mashambulizi yake ya kinyama dhidi ya nchi hiyo maskini ya Kiarabu. Kwa mujibu wa televisheni ya Al Masira, kati ya waliopoteza maisha katika hujuma ya Saudia ni watoto 2,646 na wanawake 1,922.
Aidha  muungano huo vamizi umeshazishambulia skuli, hospitali, makaazi ya raia, barabara, masoko na kambi za wakimbizi na kuua maelfu ya raia wasio na hatia wa Yemen. Ndege za kivita za Saudia aidha zimebomoa nyumba za raia zipatazo 403,039 na misikiti 712.

WENGI WAJITOKEZA KATIKA UCHAGUZI WA SAARLAND UJERUMANI KULIKO 2012

Idadi ya Wajerumani waliojitokeza kupiga kura katika uchaguzi wa jimbo dogo la magharibi la Saarland ni juu kidogo kuliko idadi ya waliojitokeza katika uchaguzi uliopita wa mwaka 2012. Hadi kufikia saa nane mchana wa leo takriban asilimia 32.6 ya wapiga kura walishapiga kura zao, tofauti na uchaguzi uliopita ambapo wakati sawa na huo, ni asilimia 31.1 ya wapiga kura ndio walikuwa wamejitokeza. Ongezeko la asilimia hiyo ndogo inatizamwa kuwa ishara za awali ya jinsi hali itakavyokuwa katika uchaguzi mkuu wa Ujerumani mwezi Septemba. Uchaguzi huo unaojiri miezi sita kabla ya uchaguzi mkuu mwezi Septemba, unatizamwa kama kipimo kinachoweza kubaini ushawishi wa Kansela Angela Merkel dhidi ya washindani wake wa siasa za wastani za mrengo wa kushoto. Uchaguzi huo ni wa kwanza miongoni mwa chaguzi tatu za majimbo zitakazofanyika kabla ya uchaguzi mkuu. Kadhalika ndio uchaguzi wa kwanza tangu Martin Schulz kuidhinishwa na chama chake cha SPD kugombea ukansela dhidi ya Merkel.

MAGAIDI WATANO WAUAWA , 16 WATIWA MBARONI KASKAZINI MWA MISRI

Wanajeshi wa Misri katika operesheni ya kupambana na mgaidi, Sinai Kaskazini
Jeshi la Misri leo limetoa taarifa na kusema kuwa, limefanikiwa kuua magaidi watano na kuwatia mbaroni wengine 16 katika operesheni maalumu iliyofanywa na jeshi hilo kaskazini mwa Misri.
Msemaji wa jeshi la Misri, Kanali Tamer el  Refae amesema, magaidi watano wakufurishaji akiwem mmoja wa viongozi wa kundi la kigaidi Baytul Muqaddas linalofanya mashambulizi yake mengi kaskazini mwa Rasi ya Sinai wameuawa kwenye operesheni hiyo. Amesema, magaidi wengine 16 wametiwa mbaroni katika opereseheni hiyo.
Kwa mujibu wa Kanali Tamer el Refae, jeshi la Misri limekamata pia kiwango kikubwa cha silaha pamoja na kutegua mabomu yaliyokuwa yametegwa na wanamgambo hao.
Magaidi wa Daesh wakijiandaa kushambulia makazi ya raia kwa roketi wanaloliita "Jahannam"

Eneo la Sinai Kaskazini huko Misri limeshuhudia mashambulizi mengi ya kigaidi tangu mwaka 2013 baada ya jeshi la nchi hiyo kufanya mapinduzi yaliyoongozwa na Rais wa hivi sasa wa Misri, Jenerali Abdul Fattah el Sisi. Mapinduzi hayo ya kijeshi yalimuondoa marakani rais wa kwanza kuchaguliwa kidemokrasia nchini Misri, Mohammad Morsi ambaye hivi sasa yuko jela. Al Arish ambayo ndiyo makao makuu ya mkoa huo wa kaskazini mwa Misri ndio mji unaoshuhudia mashambulizi mengi ya kigaidi.
Hadi hivi sasa kundi la Ansar Baytul Muqaddas limeshafanya makumi ya mashambulizi dhidi ya maeneo ya wanajeshi na raia wa kawaida wa Misri na kuua watu wengi sambamba na kuharibu miundombinu ya nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika.

IRAN KUIWEKEA MAREKANI VIKWAZO

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Iran, Is'haq Jehangiri
Kufuatia hatua ya Marekani ya kuiwekea Iran vikwazo, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nayo itachukua hatua kadhaa ikiwa ni pamoja na kuiwekea Marekani vikwazo.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Iran, Is'haq Jehangiri amesema, serikali ya Iran inachunguza hatua itakazochukua endapo Marekani itakiuka mapatano ya nyuklia yajulikanayo kama Mpango wa Pamoja wa Utekeelzwaji JCPOA.
Jehangiri amesema hata kama vikwazo vipya vya Marekani si ukiukwaji wa JCPOA, lakini Marekani itapoteza itibari yake kimataifa.
Jehangiri amesisitiza kuwa, uchumi wa Iran unazidi kuimarika kutokana na utekelezwaji wa sera za uchumi wa kimapambano na kuongeza kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa umoja na mshikamano imeweza kusimama kidete mbele ya vikwazo vikubwa  zaidi.
Hivi karibuni wajumbe kadhaa wa vyama vya Democrat na Republican katika Baraza la Senate la Marekani walipasisha rasimu ya sheria ya kushadidisha vikwazo dhidi ya Iran.
Bunge la Congress la Marekani
Kwa mujibu wa rasimu hiyo, watu na mashirika au taasisi za Iran zitawekewa vikwazo kwa kuhusika na mpango wa makombora ya kujihami ya nchi hii.
Katika kujibu hatua hiyo, Kamati ya Sera za Kigeni na Usalama wa Taifa katika Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu, Bunge la Iran, linapanga kuwasilisha mswada wa kulitaja Jeshi la Marekani na Shirika la Kijasusi la Marekani CIA kuwa taasisi za kigaidi.
Aidha katika hatua ya kujibu kufuatia uhasama na chuki za Baraza la Congress la Marekani, Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imetangaza kuyawekea vikwazo mashirika 15 ya Marekani kutokana na mashirika hayo kuunga mkono jinai na ugaidi wa utawala haramu wa Israel. Katika taarifa yake, Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imesema mashirika hayo ya Mareknai yamekiuka azimio 2334 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa kuunga mkono ugaidi wa Israel. Aidha taarifa hio imelaani muswada huo wa vikwazo vya Marekani dhidi ya Iran na kuutaja kuwa ni kinyume cha sheria za kimataifa.

UCHAGUZI WA JIMBO LA SAARLAND MTIHANI KWA MERKEL NA SCHULZ

Wajerumani katika jimbo dogo la Saarland lililoko magharibi mwa Ujerumani wanapiga kura leo Jumapili katika uchaguzi wa majimbo ambao unaonekana kuwa kipimo cha umaarufu wa Kansela wa Ujerumani Angela Merkel.
Frankreich Angela Merkel und Martin Schulz in Verdun (Getty Images/S. Gallup)
Uchaguzi wa jimbo la Saarland ndiyo wa kwanza kati ya chaguzi tatu za majimbo zitakazofanyika kabla ya uchaguzi wa huo wa Septemba 24.
Kwa maana hiyo unatoa fursa kwa vyama kujenga au kupoteza kasi katika jitihada zao za kuibuka mshindi katika ngazi ya kitaifa. Kwa sasa jimbo la Saarland linaongozwa na muungano wa chama cha kihafidhina cha Merkel CDU na chama cha msimamo wa wastani wa mrengo wa kulia Social Democrat SPD.
Matokeo ya maoni ya wanachi yaliyotolewa na kituo cha televisheni cha serikali ZDF yanaonyesha CDU ikiungwa mkono kwa asilimia 37 dhidi ya SPD inayoungwa mkono kwa asilimia 32. Chama cha di Linke kinachotarajiwa kuungana na SPD kina asilimia 12.5.
Saarland kipimo cha mambo yatakavyokuwa Septemba
Uchaguzi wa Saarland ndiyo mtihani wa kwanza kwa mgombea Ukansela wa chama cha SPD Martin Schulz ambaye amekipiga jeki chama hicho tangu kutangazwa kuwa mgombea wake dhidi ya Merkel. Schulz ameahidi kushughulikia suala la kukosekana kwa usawa, ambalo wapiga kura wengi wanalichukulia kwa uzito.
Karte Saarland Saarbrücken ENG Ramani ya Jimbo la Saarland
Licha ya kuwa jimbo hilo la Saarland liliko mpakani na Ufaransa lina wakaazi takriban milioni moja, uchaguzi wake wa leo unachukulika kuwa muhimu sana katika kupima umaarufu wa Merkel dhidi ya Schulz.
SPD imejiongezea umaarufu kwa alama 10 kitaifa tangu Schulz kutangazwa mgombea mwezi Januari akiapa kuufikisha kikomo utawala wa Merkel wa miaka 12 madarakani. Ushawishi wa Schulz umewavutia hasa wapiga kura vijana katika nyanja ya kitaifa na katika jimbo la Saarland.
Merkel aliuambia mkutano wa hadhara alipokuwa akikifanyia chama chake kampeni katika mji wa Sankt Wendel ulioko mpakani kati ya Ujerumani, Ufaransa na Luxembourg kuwa kipindi hiki kila kura ina uzito mkubwa.
Kura za maoni zinabashiri muungano wa SPD, chama cha mrengo wa kushoto cha die Linke na chama cha wanamazingira wanaoegemea mrengo wa kushoto cha kijani au muungano wa SPD na Die Linke iwapo chama cha kijani kitashindwa kupata kura za kutosha katika uchaguzi huo.
Ni CDU au SPD?
Kura nyingine ya maoni iliyotolewa wiki iliyopita inaonyesha kuwa SPD na vyama vya kihafidhina CDU na CSU vinaungwa mkono kitaifa kwa asilimia 32. Lakini kura za maoni za Deutschlandtrend zinaonya asilimia 44 ya wapiga kura wanataka SPD kuongoza serikali ijayo ikilinganishwa na asilimia 33 ya wanaotaka chama cha Merkel kuongoza.
Wahlkampf Saarland 2017 (Getty Images/S. Gallup) Mabango yanayoonesha wagombea wa Saarland
Chini ya utawala wa Merkel Ujerumani imeshuhudia kuimarika kwa uchumi wake na idadi ya walioajiriwa ikiwa juu lakini pengo kati ya matajiri na masikini imezidi kuongezeka.
Schulz rais wa zamani wa bunge la Ulaya mwenye umri wa miaka 61 anajaribu kuwavutia wapiga kura walio katika tabaka la walioajiriwa, kupitia ujumbe wa matumaini wa kuwepo usawa na haki za kijamii.
Kura za maoni zinabashiri kinyang'anyiro kikali kati ya waziri mkuu wa sasa wa Saarland Annegret Kramp Karrenbauer mwenye umri wa miaka 54, mgombea wa CDU kwa jina la utani AKK, na naibu wake Anke Rehlinger mwenye umri wa miaka 40 mgombea wa chama cha SPD.
Vituo vya kupigia kura vinafunguliwa saa mbili asubuhi na matokeo ya awali yanatarajiwa kutangazwa na vyommbo vikuu vya habari vya Ujerumani baada ya vituo kufungwa saa kumi na mbili jioni.

Tuesday, March 21, 2017

SIKU YA KIMATAIFA YA MISITU DUNIANI ILIYOYO ADHIMISHWA JANA MACHI 21, 2017

Kauli mbiu ya mwaka huu wa 2017 inasema "Misitu na Nishati" ikiwa ni mahsusi kutokana na uwekezaji mkubwa katika uvumbuzi wa teknolojia na usimamizi endelevu wa misitu kama suala muhimu.
BG Great Walks | Regenwald (picture-alliance/blickwinkel/K. Irlmeier)
Katika kuiadhimisha siku ya kimataifa ya misitu kila mwaka, nchi mbalimbali duniani zinahamasishwa kuendeleza juhudi za kitaifa na kimataifa ili kuandaa na kushiriki katika shughuli zinazohusika na misitu pamoja na miti, kama vile kampeni ya kupanda miti pamoja na midahalo kuhusu misitu. Siku hii huadhimishwa kwa ajili ya kuwafanya watu waelewe umuhimu wa aina zote za misitu duniani, ikiwemo jukumu lake katika mabadiliko ya tabia nchi.
Uwekezaji na usimamiizi endelevu wa misitu
Kwa mujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO, kaulimbiu ya mwaka huu ya 'Misitu na Nishati', imechaguliwa kutokana na uwekezaji mkubwa katika uvumbuzi wa teknolojia na katika usimamizi endelevu wa misitu kuwa suala muhimu katika kuongeza nafasi ya misitu kama chanzo kikuu cha nishati mbadala.
Wangari Maathai (AP) Mwanaharakati wa mazingira kutoka nchini Kenya ambaye sasa ni marehemu Wangari Maathai
Kulingana na suala hilo, uwekezaji sasa unaangaziwa zaidi katika mustakabali endelevu ili kufikia Malengo ya Maendeleo Endelevu na kukuza uchumi wa kijani. Kwa mujibu wa FAO, kuongezeka kwa kaya na jamii yenye vitalu vya miti pamoja na matumizi ya majiko ya kutumia kuni, kunaweza kuwapatia mamilioni ya watu zaidi katika nchi zinazoendelea urahisi wa kupatikana kwa nishati mbadala ambayo ni nafuu na yenye kuaminika. 
Maadhimisho ya mwaka huu
Shirika la FAO litaiadhimisha siku hii katika makao makuu ya shirika hilo mjini Roma, Italia, ambapo mkurugenzi wake mkuu, Jose Graziano da Silva, atafungua maadhimisho hayo. Miongoni mwa mada zitakazojadiliwa katika maadhimisho haya ni pamoja na majukumu ya misitu na nishati ya kijani katika utekelezaji wa makubaliano ya Paris ya Nationally Determined Contributions, NDCs, ambayo itatolewa na Rais wa Jamhuri ya Fiji, Jioji Konusi Konrote.
Afghanistan Provinz Kunar - Holzwirtschaft und Produktion (DW/O. Deedar) Ukutaji wa miti kwa ajili ya matumizi mbalimbali ni chanzo kikubwa cha uharibifu wa misitu
Aidha, Katibu Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kupambana na Kuenea kwa Jangwa, UNCCD, Monique Barbut, atatoa mada kuhusu suala la kufungamana kwa misitu na nishati, ambalo ni suala muhimu la maendeleo endelevu pamoja na ushujaa katika maisha ya watu. Eva Müller, Mkurugenzi wa Idara ya Sera za Misitu na Ugavi wa Rasilimali katika shirika la FAO, atazindua chapisho la FAO ambalo linazungumzia kipindi cha mpito cha matumizi ya mkaa: thamani ya mkaa katika kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na kuimarisha maisha ya watu.
Aidha, Müller atatoa mada kuhusu ajenda inayochukuliwa na FAO katika misitu na nishati ya kijani. Naye Makamu wa Rais wa shirika la Metsa, Rikka Joukio, atatoa mada kuhusu mustakabali wa nishati katika jamii katika kuuvumbua mtazamo huo. Maadhimisho hayo yatahitimishwa kwa hotuba itakayotolewa na Maria Helena Semedo, Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Hali ya Hewa na Maliasili wa FAO.
Siku hii ilianzishwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mwaka 2012 na siku hiyo ilisherehekewa kwa mara ya kwanza Machi 21, 2013.

Friday, March 17, 2017

TRUMP ASEMA KOREA KAZKAZINI INAJIENDESHA VIBAYA SANA NA CHINA HAISAIDII

Rais wa Marekani Donald Trump ameilezea tabia ya Korea Kaskazini kuwa ni mbaya sana, na kuishtumu China kwa kutofanya vya kutosha kusaidia kubadili mwenendo wa taifa hilo ambalo ni mshirika wake wa karibu. Kauli ya Trump inakuja saa chache baada ya waziri wake wa mambo ya nje Rex Tillerson kusema hatua za kijeshi dhidi ya Korea Kaskazini ni jambo ambalo wanalizingatia baada ya kuonya kuwa sera ya uvumilivu wa kimkakati juu ya Korea Kaskazini imekwisha. Tillerson ambaye yuko ziarani Korea Kusini anatarajiwa kuizuru China hapo kesho na siku ya Jumapili atakutana na Rais wa China Xi Jinping.

KANSELA WA UJERUMANI ANGELA MERKEL KUKUTANA NA DONALD TRUMP

Kansela wa Ujerumani Angela Merkel anatarajiwa kukutana na rais wa Marekani Donald Trump kwa mara ya kwanza mjini Washington. Mazungumzo yao yatajikita juu ya sera yenye utata ya Rais Trump ya 'Marekani kwanza',  
Angela Merkel und Donald Trump (picture-alliance/dpa/M. Kappeler/R. Sachs)
Kansela wa Ujerumani Angela Merkel na mwenyeji wake rais Donald Trump wanatarajiwa kujadili uhusiano baina ya nchi zao na juu ya uhusiano kati ya Marekani na Umoja wa Ulaya kama mshirika wa Marekani katika biashara, usalama na maadili ya kimsingi.  Kwa mujibu wa duru za serikali ya Ujerumani Kansela Merkel pia anataka kujadili na mwenyeji wake, migogoro ya Syria, Libya, hali ya nchini Afghanistan na mgogoro wa nchini Ukraine. Maswala mengine ni uhusiano na Urusi, harakati za kupambana na ugaidi na sera juu ya wakimbizi.  Hata hivyo wachunguzi wanasema huenda swala jingine muhimu likawa msimamo wa rais Donald Trump juu ya kuyaweka mbele maslahi ya nchi yake na mtazamo wake juu mikataba ya biashara na jinsi inavyohusiana na uchumi wa Marekani. 
Mwakilishi wa Ujerumani anayesimamia kamati ya Ulaya inayoshughulikia uhusiano na nchi za nje Josef Janning amesema siasa za Marekani hazijawahi kuwa za kutatanisha kama ilivyo sasa.  Kwa upande wake Profesa John Harper wa chuo kikuu cha Johns Hopkins cha Bolgna na mtaalamu wa sera za nje za Marekani amesema kansela Merkel atapaswa kutafuta njia mpya ya kujaribu kuanzisha uhusiano wa kikazi na rais Trump. Profesa huyo amesema rais Trump anatofautiana sana na marais wa Marekani wa hapo awali Barack Obama na George Bush kwa sababu Trump hakuwa na uzoefu wa kuendesha  serikali kabla ya kuwa rais.
Deutschland Angela Merkel, Spitzengespräch der deutschen Wirtschaft in München (picture-alliance/Geisler-Fotopress) Kansela wa Ujerumani Angela Merkel
Viongozi hao wanatofautiana sana katika mitazamo ya siasa za dunia; kwa mfano Kansela anapendelea ushirikiano na nchi nyingine katika kuzikabili siasa za dunia wakati Trump kama anavyoendelea kubainika anaonyesha kupendelea mtazamo wa taifa kubwa katika kuyakabili maswala ya kimataifa. Trump anapuuza ushirikiano na taasisi za kimataifa na badala yake anazingatia siasa kwa mtazamo wa mashindano.
Bwana Josef Janning amesema lengo la Kansela Merkel ni kupata angalau kauli thabiti ya rais Trump juu ya mchakato wa nchi zilizoendelea kiviwanda na zile zinazoinukia kiuchumi  G-20 na juu ya haja ya kuyashughulikia maswala kwa njia ya ushirikiano. Naye Profesa Harper anasema anatumai kuwa Kansela Merkel atafanikiwa kumshawishi rais Trump aache kuushutumu Umoja wa Ulaya na pia aache kuwaendekeza wanasiasa kama Marine le Pen wa Ufaransa. Ni vigumu kubainika katika mkutano wa kwanza wa viongozi wa Ujerumani na Marekani iwapo watakubaliana msingi wa kufanya kazi kwa pamoja. Hata hivyo kansela wa Ujerumani aliliambia gazeti moja la hapa nchini Ujerumani "Saarbruecker" kwamba wakati wote ni vizuri kujadiliana badala ya kumjadili mtu. Bibi Merkel amesema Ujerumani na Marekani zitanufaika ikiwa zitashirikiana vizuri na kwa haki.

EU YATAKA UFANYIKE UCHAGUZI WA KIMATAIFA KUHUSU UNYAMA WALIOFANYIWA WAISLAMU WAROHINGYA

Umoja wa Ulaya (EU) umetaka Umoja wa Mataifa uanzishe uchunguzi kuhusu mateso, ubakaji na mauaji yaliyofanywa dhidi ya jamii ya wachache ya Waislamu Warohingya nchini Myanmar.
Rasimu ya azimio ambayo Umoja wa Ulaya umeiwasilisha kwenye Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa hapo jana la kuanzishwa uchunguzi wa kimataifa nchini Myanmar imetumia lugha kali zaidi kuliko rasimu inayofanana na hiyo iliyowasilishwa na EU hapo kabla.
Ripoti ya mwezi uliopita ya Umoja wa Mataifa iliyoandaliwa kulingana na ushahidi uliotolewa na manusura waliokuweko nchini Bangladesh inaonyesha kuwa jeshi na polisi ya Myanmar wametenda jinai dhidi ya Waislamu wa jamii ya wachache ya Rohingya kwa namna ya kuangamiza kizazi na jinai dhidi ya binadamu.
Waislamu Warohingya wanaoteseka nchini Myanmar
Aidha itakumbukwa kuwa ripoti iliyotolewa na shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch imeeleza kuwa kwa akali nusu ya wanawake na mabinti 101 wa Kiislamu wa jamii ya Rohingya waliohojiwa na Ofisi ya Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa walisema kuwa, walibakwa na kunajisiwa na askari wa serikali ya Myanmar.
Tarehe 23 na 24 za mwezi huu wa Machi, Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa linatazamiwa kuipigia kura rasimu ya azimio lililorejeshwa tena mbele ya baraza hilo kuhusu hali ya Waislamu wa Rohingya nchini Myanmar.
Umoja wa Mataifa umewataja Waislamu wa Myanmar kuwa jamii ya wachache inayokandamizwa zaidi dunaini..

SERIKALI YA SUDAN KUSINI YALAUMIWA KWA KUSABABISHA BAA LA NJAA

Serikali ya Sudan Kusini ndiyo inayobeba lawama kubwa kwa baa la njaa linaloshuhudiwa katika baadhi ya sehemu za nchi hiyo iliyoharibiwa na vita.
Hayo yamesemwa na Umoja wa Mataifa katika kipindi hiki ambapo mgogoro wa kibinadamu unaoisumbua nchini huyo unakaribia kuwa maafa makubwa ya kibinadamu. 
Ripoti iliyotolewa na Umoja wa Mataifa imesema: Serikali ya Sudan Kusini ndiyo inayobeba lawama kubwa kwa baa la njaa linaloshuhudiwa katika baadhi ya sehemu za nchi hiyo huku Rais wa nchi hiyo Salva Kiir akiendelea kutumia mamilioni ya dola zinazotokana na mauzo ya mafuta kuimarisha vikosi vyake vya ulinzi.
Umoja wa Mataifa unasema baadhi ya maeneo ya Sudan Kusini yanakabiliwa na baa la njaa na kwamba karibu nusu ya jamii ya watu wa nchi hiyo yaani karibu watu milioni tano na laki tano, wanasumbuliwa na uhaba wa chakula. 
Raia wanaosumbuliwa na njaa Sudan Kusini
Ushahidi unaonesha kuwa, baa hilo la njaa linatokana na machafuko na vita hususan katika jimbo la Unity, hatua ya jeshi la serikali ya kuwazuia watoa misaada ya kibinadamu kufika kwenye maeneo yenye njaa na kukimbia raia kutokana na mapigano ya ndani. Umoja wa Mataifa unasema kwa uchache nusu ya raia wa Sudan Kusini wamelazimika kuwa wakimbizi katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita. 
Sudan Kusini ilitumbukia katika vita vya wenyewe kwa wenyewe mwaka 2013 baada ya Rais Salva Kiir wa nchi hiyo kumtuhumu aliyekuwa makamu wake, Riek Machar kuwa alifanya jaribio la mapinduzi. Japokuwa makubaliano ya amani yaliyotiwa saini mwaka 2015 yalizidisha matumaini ya kuhitimishwa vita vya ndani lakini machafuko yanayoendelea katika maeneo mbalimbali ya nchi hiyo yamezusha tena wasiwasi mkubwa na kusababisha matatizo mengi kwa raia wa kawaida. Makubaliano hayo ya amani pia yamefutiliwa mbali baada ya kiongozi wa  waasi, Riek Machar kukimbilia nje ya nchi.
Hata hivyo kukimbia kwa Machar hakukuhitimisha vita vya ndani nchini Sudan Kusini na ripoti mbalimbali zinasema jeshi linalodhibitiwa na Rais Salva Kiir limekuwa likifanya mauaji ya kikabila. Ripoti ya Umoja wa Mataifa pia imethibitisha kuwa, mauaji ya kimbari yanafanyika nchini Sudan Kusini lakini hadi sasa hakujachukuliwa hatua madhubuti za kukomesha hali hiyo.
Salva Kiir na Riek Machar
Sambamba na hayo Sudan Kusini inasumbuliwa na matatizo makubwa ya kiuchumi. Mamilioni ya raia wanaishi kama wakimbizi katika maeneo ya mpakani au kwenye nchi jirani, na wengi miongoni mwao wanasumbuliwa na uhaba wa chakula na huduma za afya. Mashamba ya kilimo yameharibika na wakulima wengi wanalazimika kuishi katika kambi za wakimbizi.
Takwimu zinaonesha kuwa, sasa asilimia 42 ya watu wote wa Sudan Kusini wanakabiliwa na baa la njaa kutokana na matatizo hayo ya kiuchumi, vita vya ndani na kusambaratika kwa sekta ya kilimo.
Mgogoro wa Sudan Kusini kwa upande mwingine unachochewa zaidi na uingiliaji wa madola ya kigeni ambayo yananyonya maliasili na utajiri wa nchi hiyo changa zaidi barani Afrika. Pato la mafuta la nchi hiyo sasa linatumika kununua silaha kutoka kwa makampuni makubwa ya nchi za Magharibi ambazo hapana shaka kuwa hazitaki au kwa uchache hazipendelei kuona soko la silaha za zana za kivita la Sudan Kusini likitoweka kwa kupatikana amani na utulivu nchini humo. 
Jeshi la Sudan Kusini linatuhumiwa kufanya mauaji ya kimbari
Ni kweli kwamba kwa sasa nchi kadhaa za Afrika zinasumbuliwa na baa la njaa, lakini pia hatuwezi kukanusha kwamba, utendaji mbaya wa viongozi wa Sudan Kusini umechangia sana katika kuzidisha hali mbaya ya sasa nchini humo. Baya zaidi ni kuwa, viongozi wa Serikali ya Sudan Kusini wanawazuia wafanyakazi wa jumuiya ya misaada ya kibinadamu kufika katika baadhi ya maeneo ya nchi hiyo.
Kwa msingi huo inathibitika kuwa, mgogoro wa sasa wa Sudan Kusini ni matokeo ya siasa mbaya za viongozi wa nchi hiyo zinazosababisha maafa makubwa kwa raia wa kawaida, na jamii ya kimataifa inalazimika kuchukua hatua madhubuti zaidi za kukabiliana na viongozi kama hao wasiowajibika. 

SHAMBULIO LA ANGA LA MAREKANI LAUA WATU 42 NA KUJERUHI 100 MSIKITINI SYRIA

Raia wasiopungua 42 wameuawa katika shambulio la anga la jeshi la Marekani lililolenga msikiti uliojaa waumini ndani yake karibu na mji wa Halab (Aleppo) kaskazini mwa Syria. Watu wengine zaidi ya 100 wamejeruhiwa katika shambulio hilo lililofanywa katika kijiji cha al-Jineh kilichopo kilomita 30 magharibi mwa mji wa Halab.
Kwa mujibu wa ripoti ya kanali ya televisheni ya Press TV shambulio hilo lililotokea usiku wa kuamkia leo lilifanyika huku watu wapatao 300 wakiwa wamo ndani ya msikiti huo.
Abu Muhammad, ambaye ni mmoja wa wanakijiji amesema alisikio mlio mkubwa wa mripuko wakati msikiti huo ulipolengwa, mara baada ya sala ambapo kwa kawaida hufanyika darsa za wanaume msikitini humo.
Ndege za kivita za Marekani
Kwa mujibu wa ripoti, watu wengi walikuwa wangali wamekwama ndani ya msikiti huo ulioporomoka huku waokoaji wakijaribu kuwafukua na kuwatoa manusura kwenye vifusi.  
Katika taarifa yake, jeshi la Marekani limedai kuwa ndege za kivita za nchi hiyo ziliwalenga viongozi wa mtandao wa kigaidi wa Al-Qaeda. Hii ni katika hali ambayo kwa mujibu wa ripoti, jengo linalodaiwa kufanyika ndani yake kikao cha wanachama wa kundi hilo la kigaidi lipo umbali wa mita 15 tu kutoka msikiti ulioshambuliwa na ndege za Marekani.
Kamandi ya jeshi la Marekani aidha imetangaza kuwa itachunguza ripoti kwamba katika shambulio hilo ulilengwa msikiti na watu kadhaa wameuawa…

Friday, March 10, 2017

MAJIBU YA CHINA DHIDI YA RIPOTI YA HAKI ZA BINADAMU ILIYOTOLEWA NA MAREKANI

China imejibu ripoti ya Marekani iliyoituhumu nchi hiyo kuwa inakiuka haki za na kuitaja Marekani kuwa ndiyo mkiukaji mkubwa zaidi wa haki za binadamu duniani.
Ripoti iliyotolewa na China imesema hali ya haki za binadamu nchini Marekani inasikitisha mno.
Ijumaa ya jana Baraza la Serikali ya China lilijibu ripoti ya haki za binadamu iliyotolewa mwaka jana 2016 na Marekani dhidi yake. Ripoti ya Baraza la Serikali ya Uchina imesema kuwa, Marekani si tu kwamba haizingatii mipaka ya haki za binadamu ndani ya nchi, bali hata nje ya nchi hiyo inakanyaga wazi wazi haki hizo.
Wafungwa waliofurika katika jela za Marekani
Hii si mara ya kwanza ambapo Marekani imekuwa ikiandaa ripoti mbalimbali dhidi ya China ikiituhumu kuwa inakandamiza na kukanyaga haki za binadamu. Watayarishaji wa ripoti ya Baraza la Serikali ya China wanasema kuwa, Marekani inashika nafasi ya pili kwenye orodha ya nchi zinazoongoza kwa kuwa na wafungwa wengi duniani na kila kati ya watu laki moja wa jamii ya Marekani, 693 wamefungwa jela. Aidha kati ya kila raia wawili wa Marekani, mmoja wao anamiliki silaha ya moto. Ripoti hiyo imeeleza kuwa, zaidi ya kesi elfu 58 za hujuma za silaha za moto zimeripotiwa, ambapo kati ya hizo watu 385 wameuawa kwa silaha hizo.
Sehemu ya wafungwa waliokata tamaa ya maisha huko Marekani
Ukweli ni kwamba, Marekani hakuna haja ya kurejea kwenye takwimu zilizotolewa katika ripoti ya Baraza la Serikali ya China ili kutambua ukiukwaji mkubwa wa  haki za binadamu unaofanyika nchini humo. Hivi karibuni Rais wa 45 wa Marekani, Donald Trump ambaye aliyekuwa akihutubia Bunge la Kongresi la nchi hiyo aliweka wazi uhalisia uliofichika katika siasa za Marekani. Trump alijikita katika kuzungumzia migogoro mikubwa ya kijamii, kiuchumi na tofauti kubwa ya kitabaka kati ya walio nacho na wasiokuwa nacho nchini Marekani na kusema kuwa, uwepo wa watu milioni 49 wasio na ajira, kusambaratika viwanda elfu 60, uwepo wa watu milioni 43 wanaosumbuiwa na njaa, kuchaa kwa miundombinu, uwepo wa magenge ya uhalifu yanayofanya magendo ya dawa za kulevya na hatimaye kuenea ukatili na chuki nchini humo ni kati ya jinai zinazoshuhudiwa sana dhidi ya haki za raia.
Ukandamizaji wa polisi wa Marekani dhidi ya raia
Uchina kama nchi inayoongozwa na mfumo wa chama kimoja kwa zaidi ya miongo sita sasa inaonekana katika fikra za walio wengi kama nchi yenye aina fulani ya udikteta wa kisiasa,. Hata hiyo ukweli ni kwamba, baada ya Vita vya Pili vya Dunia Marekani iliimarisha nafasi yake kwa kutumia taasisi kama vile NATO, Benki ya Dunia na Mfumo wa Fedha wa Kimataifa (IMF). Marekani imezivamia zaidi ya nchi 60 za dunia, kupindu na kuondoa madarakani makumi ya serikali huru, kuanzisha kambi 800 za kijeshi katika maeneo mbalimbali ya dunia kwa gharama sawa na asilimia 35 ya bajeti yote ya kijeshi ya dunia, mambo ambayo yanaidhihirishia dunia kuwa nchi hiyo ndiye msababishaji wa migogoro ulimwenguni. Jambo lisilo na shaka ni kuwa Donald Trump hatofautiani na marais waliomtangulia wa Marekani.
Mateso yaliyopigwa marufuku na UN yangali yanafanywa na askari wa Marekani dhidi ya watuhumiwa
Uchina inaamini kuwa, katika miaka ya hivi karibuni, Marekani imekuwa ikipotosha fikra za walio wengi kuhusiana na suala zima la utetezi wa demokrasia na haki za binaadamu duniani. Uvamizi wa kijeshi wa nchi hiyo huko Iraq na Afghanistan, unabainisha wazi sera za kindumakuwili na hadaa nyingi za Washington kwa walimwengu. Kadhalika sera za kuingilia mambo ya nchi nyingine zinazotekelezwa na Marekani huko katika nchi za Amerika ya Latini ni kati ya hatua nyingine za watawala wa Washington kwa lengo la kutaka kuziondoa madarakani serikali huru za mataifa hayo. Swali la msingi ni kwamba, kwa kuwa na historia hii, Marekani inaweza kuwa na ustahiki wowote wa kuongoza dunia?
Polisi wa Marekani akimuadhibu kwa mateke mwanamke asiye na silaha wala ulinzi
Je kwa mazingira uharibifu mkubwa wa Marekani katika uwanja wa kukiuka haki za binadamu za mamilioni ya watu duniani wakiwemo hata raia wake yenyewe, Washington inaweza kuwa mtetezi wa aki hizo na kuwa mwamuzi na msimamizi wa masuala ya haki za binadamu duniani?
Ni kwa kuzingatia hayo yote ndio maana China ikaitaka Marekani, badala ya kuingilia masuala ya ndani ya nchi nyingine, ishughulikie kwanza tatizo la ukosefu makazi la mamilioni ya Wamarekani, kuongezeka raia wa nchi hiyo wanaokabiliwa na njaa sambamba na kukosa huduma muhimu za kimaisha. China inaamini kuwa suala la haki za binadamu linatumiwa na Marekani kama wenzo na fimbo ya kuhalalisha sera za serikali ya Washington za kuingilia mambo ya ndani ya nchi nyingine duniani.

RIPOTI: WATOTO KARIBU MILIONI 2 WANAKUFA KILA MWAKA KWA KUVUTA HEWA CHAFU

Kwa akali watoto milioni 1.7 wanapoteza maisha kila mwaka kutokana na kuvuta hewa chafu kote duniani.
Ripoti mpya ya Shirika la Afya Duniani (WHO) imefafanua kuwa, kiwango hicho ni sawa na asilimia 25 ya vifo vya watoto wadogo walio na umri wa chini ya miaka mitano kote duniani.
WHO imebainisha kuwa, mazingira machafu, hewa na maji machafu pamoja na moshi wa sigara yanasababisha robo ya vifo vya watoto wadogo kote duniani kila mwaka.
Watoto wadogo, wahanga wakuu wa hewa chafu
Margaret Chan, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani amesema kuwa, hewa na maji machafu yamechangia watoto wengi kupatwa na maradhi ya pumu, malaria, kutapika na kuendesha, magonjwa ambayo yanaongoza kwa vifo vya watoto wadogo duniani.
Mwaka jana 2016, Shirika la Afya Duniani (WHO) lilionya kuwa hali ya uchafuzi wa hewa inazidi kuwa mbaya duniani kote huku zaidi ya asilimia 80 ya wakaazi wa miji mikubwa wakivuta hewa chafu na kuongeza hatari ya kupatwa na saratani ya mapafu na maradhi mengine hatari.

SERIKALI YA LEBANON: TUNAHITAJI SANA HIZBULLAH KWA AJILI YA ULINZI WA NCHI

Waziri Mshauri katika Masuala ya Ikulu ya Rais wa Lebanon, amesema kuwa nchi hiyo inaihitajia sana Harakati ya Hizbullah kwa ajili ya kukabiliana na kuzuia hujuma za utawala haramu wa Israel na makundi ya kigaidi dhidi ya ardhi ya nchi hiyo.
Sambamba na kusisitizia nafasi chanya ya harakati hiyo ya muqawama, Pierre Raffoul amesema kuwa, hata katika sherehe za kuapishwa Rais Michel Aoun alisema kuwa, silaha za Hizbullah si tu kwamba zinasaidia katika kusimamia usalama ndani ya nchi, bali hata nje ya mipaka ya Lebanon, zinahusika pia katika kuzuia chokochoko za Israel na makundi ya kigaidi. 
Pierre Raffoul, Waziri Mshauri katika Masuala ya Ikulu ya Rais wa Lebanon
Akifafanua kuwa silaha zinazotumiwa na Hizbullah ni silaha zinazotumiwa na jeshi la Lebanon, Raffoul amesema kuwa, ni silaha hizo hizo zilizoweza kuupigisha magoti utawala wa Kizayuni katika vita vya mwaka 2006. Itakumbukwa katika katika vita vya siku 33, mwaka 2006 kati ya utawala wa Kizayuni wa Israel na Lebanon, Israel ilishindwa vibaya ambapo kutokana na kupata hasara kubwa, ililazimika kurudi nyuma na kusalimu amri. 
Wanamapambano shupavu wa harakati ya Hizbullah ya Lebanon, wanaoitia kiwewe Israel na Marekani
Hivi karibuni Rais Michel Aoun akihojiwa na televisheni ya CBC na gazeti la Misri la al-Ahram alisema kuwa, anaonga mkono kuendelea ushirikiano wa harakati ya Hizbullah na jeshi la Lebanon, udharura wa kulindwa silaha za harakati hiyo na uwepo wa Hizbullah nchini Syria katika vita dhidi ya makundi ya kigaidi na ukufurishaji ili kulinda taifa la Lebanon.
Aidha hivi karibuni Alexander Zasypkin, balozi wa Russia nchini Lebanon alisema kuwa, tangu awali harakati ya Hizbullah imekuwa na nafasi muhimu na chanya katika kupambana na magaidi nchini Syria na kudumisha usalama nchini Lebanon.

UN YATAKA KUTUMWA ASKARI WENGINE WA KIMATAIFA DRC

António Guterres, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amelitaka Baraza la Usalama la umoja huo kutuma askari wengine 320 wa kofia buluu huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
António Guterres alitoa mwito huo jana Ijumaa kwenye ripoti yake kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na sambamba na kuelezea kusikitishwa sana na kuongezeka uvunjaji wa haki za binadamu nchini humo, ametaka kuongezewa nguvu kikosi cha kimataifa cha kulinda amani MONUSCO ili kiweze kuwa na uwezo mkubwa zaidi wa kuwalinda raia.
Katika ripoti yake hiyo, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa aidha ametaka vikosi vingine viwili vitumwe katika miji ya Lubumbashi na Katanga ili kuzuia miji hiyo kukumbwa na machafuko wakati wa uchaguzi ujao.
Aidha amesisitiza kuwa, mwaka 2017 ni mwaka muhimu mno kwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Kikosi cha kulinda amani wa Umoja wa Mataifa DRC

Amesema, kikosi cha MONUSCO kinafanya kazi kubwa nchini humo na inabidi kiendelee kuwepo kwa ajili ya kusimamia mchakato wa kisiasa na kulinda mafanikio yaliyopatikana hadi hivi sasa katika jitihada za kurejesha amani na utulivu nchini humo.
Kazi kuu ya askari wa Umoja wa Mataifa nchini Kongo ni kuwalinda raia na wako nchini humo tangu mwaka 1992 chini ya mwavuli wa kikosi cha MONUSCO ambacho hivi sasa kina takriban wanajeshi 19 elfu wa kofia buluu kutoka nchi mbalimbali duniani.

Thursday, March 9, 2017

MAJIMBO KADHAA MAREKANI YACHUKUA HATUA KUZUIA MARUFUKU MPYA YA TRUMP DHIDI YA WAISLAMU

Amri mpya iliyotolewa na Rais Donald Trump wa Marekani ya kupiga marufuku raia wa nchi sita za Waislamu kuingia nchini humo imeendelea kupingwa kisheria na majimbo ya nchi hiyo baada ya Mwanasheria Mkuu wa jimbo la Washington kuungana na jimbo la Hawaii kuchukua hatua ya kuzuia utekelezaji wake.
Mwanasheria Mkuu wa jimbo la Washington Bob Ferguson, ambaye alikuwa mtu wa mwanzo kukwamisha amri ya marufuku ya kwanza iliyotangazwa na Trump amesema, amri mpya ya sasa pia inakiuka Katiba ya Marekani kwa kuwa "haiutendei ipasavyo Uislamu".
Amesema hoja iliyowasilishwa na ofisi yake inataka zuio dhidi ya amri ya mwanzo iliyotangazwa na rais wa Marekani mnamo mwezi Januari litekelezwe pia kuhusiana na dikrii yake mpya.
Hii ni katika hali ambayo Wanasheria Wakuu wa majimbo ya New York, Massachusetts na Oregon wametangaza kuwa nao pia wameshachukua hatua ya kujiunga na shauri la kisheria lililowasilishwa mahakamani na jimbo la Washington pamoja na Minnesota kupinga marufuku iliyotangazwa na Trump.
Mwanasheria Mkuu wa jimbo la Washington, Bob Ferguson
Amri hiyo mpya iliyotangazwa siku ya Jumatatu baada ya kufanyiwa marekebisho na ambayo inatarajiwa kuanza kutekelezwa tarehe 16 mwezi huu inapiga marufuku kutoa viza za kuingia Marekani watu wanaotoka Syria, Iran, Somalia, Libya, Sudan na Yemen na kufunga kwa muda wa siku 120 mpango wa Marekani kwa ajili ya wakimbizi.
Mwanasheria Mkuu wa Oregon Ellen Rosenblum amesema amri hiyo ya Rais wa Marekani imeathiri jimbo hilo, wakaazi wake, waajiri, taasisi za elimu, mfumo wa huduma za afya pamoja na uchumi.
Mwanasheria Mkuu wa jimbo la New York Eric Schneiderman amesema, kwa jina jingine amri hiyo ni "marufuku dhidi ya Waislamu"
Shauri la kisheria lililowasilishwa na jimbo la Hawaii limeeleza kuwa amri ya Trump itaathiri jamii ya Waislamu wa jimbo hilo, utalii pamoja na wanafunzi wa kigeni…/

MAREKANI YAITANGAZIA DUNIA VITA VYA KIBIASHARA

Marekani imetoa tishio la vita vya kibiashara dhidi ya dunia. Waziri wa Biashara wa Marekani Wilbur Ross amesema Marekani imekuwa katika vita vya kibiashara kwa miongo kadhaa lakini sasa nchi hiyo iko tayari kutumia uwezo wake wote kujibu mapigo.
Hivi sasa uchumi wa Marekani unakabiliwa  na nakisi ya bajeti ya takribani dola bilioni 800  huku mlingano wa kibiashara ukiwa ni kwa faida ya madola ya kigeni. Mwaka 2014, kwa kila dola  trilioni moja na bilioni 500 ambazo ni thamani ya mauzo ya nje ya Marekani, nchi hiyo imekuwa ikinunua huduma na bidhaa kutoka nje zenye thamani ya trilioni mbili na dola bilioni 300.
Katika mlingano wa mabadilishano ya kibiashara, China inaiongoza Marekani kwa dola bilioni 340, Umoja wa Ulaya bilioni 142, Japan bilioni 167, Mexico bilioni 53 na Canada bilioni 35. Kwa msingi huo nchi hizo zinauiuzia Marekani bidhaa na huduma zaidi ya Marekani inavyoweza kuziuzia.
Kiu isiyokwisha ya Wamarekani ya kutaka kutumia kwa wingi bidhaa kiholela ni jambo ambalo limepelekea nchi hiyo kukumbwa na wimbi la mmiminiko wa bidhaa za kigeni. Halikadhalika gharama za uzalishaji bidhaa Marekani ziko juu sana ikilinganishwa na maeneo mengine ya dunia; na ni kwa sababu hii ndio maana Wamarekani wanafadhilisha kununua bidhaa za kigeni ambazo zinauzwa kwa bei nafuu.
Bidhaa zikiwasili bandarini
Sheria ngumu za kuajiri wafanyakazi pamoja na mfumo mbaya wa ushuru ni mambo ambayo yamepelekea wazalishaji bidhaa Marekani kutoweza kushindana na wenzao wa kigeni.
Takwimu zinaonyesha kuwa, Marekani ndio nchi yenye uchumi mkubwa duniani na moja ya nchi muhimu zaidi kiviwanda. Pamoja na hayo miongoni mwa sekta 11 muhimu za kiviwanda, Marekani imeweza kufanikiwa katika sekta tatu tu ambazo ni sekta ya dawa, sekta ya plastiki na sekta ya utengenezaji ndege. Katika upande wa pili Marekani inaagiza kutoka nchi zingine duniani bidhaa muhimu kama vile bidhaa za elektroniki, mashine za viwanda, magari na petroli na hivyo kupelekea uchumi wa nchi hiyo kudhoofika.
Hivi sasa kwa kuzingatia matatizo katika muundo wa kiuchumi wa Marekani na uraibu wa kutumia bidhaa kupindukia (consumerism) walionao raia wa nchi hiyo, wakuu wa Washington sasa wanataka kuanzisha vita vya kibiashara na mataifa mengine duniani.
Katika miaka ya nyuma, Marekani pia ilikuwa na ushindani mkubwa na baadhi ya washirika wake wa kibiashara hasa Japan na China. Hivi sasa serikali ya Marekani imeweka kando udiplomasia na imetangaza wazi vita vya kibiashara. Hivi sasa mbali na matokeo tarajiwa ya vita vya kibiashara baina ya madola makubwa duniani, nukta nyingine muhimu ni kuwa, Marekani haiwezi kuibuka mshindi hadi pale itakapo badilisha muundo wake wa kiuchumi na kuweza kudhibiti utamaduni mbovu wa watu wake kutumia bidhaa kiholela na kupita kiasi.
Tab'an Rais Donald Trump amechukua hatua kuekelea katika marekebisho hayo kwa kutoa nara kama vile 'Marekani Ipewe Kipaumbele', 'Nunua Bidhaa za Marekani' , 'Ajiri Mmarekani' n.k. Lakini kuna shaka kubwa iwapo wazalishaji bidhaa, wafanya biashara wakubwa na raia wa Marekani  wataafiki kutekeleza mabadiliko hayo. Ni kwa sababu hii ndio maana badala ya serikali ya Marekani kujikita katika kuleta mabadiliko ndani ya nchi imechukua mkondo wa kuibua utata katika uchumi na biashara ya kimataifa kwa kutumia mabavu ili kujaribu kuzuia kuporomoka kusikoepukika kwa nchi hiyo katika uga wa kimataifa.

SILAHA ZA NYUKLIA ZA UTAWALA WA KIZAYUNI NI TISHIO KWA USALAMA WA DUNIA

Mwakilishi wa kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) amesema silaha za nyuklia za utawala wa Kizayuni wa Israel ni tishio kwa amani na usalama wa kimataifa na ametaka wakala huo uchunguze na kufuatilia kwa uzito mkubwa mpango wa silaha za nyuklia wa utawala huo.
Reza Najafi ametoa wito huo jana katika siku ya mwisho ya kikao cha msimu cha Bodi ya Magavana wa IAEA, ambapo mbali na kuashiria jinsi nchi wanachama wa Harakati Isiyofungamana na Siasa za Upande Wowote (NAM) zilivyolaani vikali mpango wa silaha za nyuklia wa utawala wa Kizayuni, ametaka suala hilo lizingatiwe kwa makini na kufuatiliwa kwa uzito mkubwa na Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki.
Najafi ameashiria wito uliotolewa mara kadhaa na jamii ya kimataifa kupitia maazimio ya IAEA na mikutano ya kuangalia upya Mkataba wa Kuzuia Uundaji na Uenezaji Silaha za Nyuklia (NPT) wa kuutaka utawala haramu wa Israel ujiunge haraka na mkataba huo na kuweka vinu vyake vya nyuklia chini ya usimamizi na uangalizi kamili wa IAEA na kueleza kuwa, kwa masikitiko, katika miaka yote hii utawala wa Kizayuni, kwa kupuuza wito wa kisheria wa jamii ya kimataifa na kwa uungaji mkono kibubusa wa baadhi ya nchi za Magharibi umeendelea kukiuka waziwazi sheria na kaununi zote za kimataifa na kuendeleza mipango yake ya kijeshi ya nyuklia.
Rais wa Marekani Trump na Waziri Mkuu wa Israel Netanyahu
Mwakilishi wa kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) amekosoa vikali pia tabia ya kindumakuwili ya baadhi ya nchi za Magharibi kuhusiana na kuzuia ueneaji wa silaha za nyuklia na katika kutekeleza marufuku kamili ya kutoipatia Israel zana na mada za nyuklia, utawala ambao kutokana na historia yake iliyojaa vitendo vya uvamizi, ukaliaji ardhi kwa mabavu na ugaidi wa kiserikali, ni tishio kwa amani na usalama wa dunia.../ 

Sunday, March 5, 2017

ISRAEL IMEWATIA NGUVUNI WAPALESTINA 420 MWEZI FEBRUARI

Ripoti mpya zinaonyesha kuwa askari wa utawala wa Kizayuni wa Israel wamewatia nguvuni na kuwaweka kizuizini Wapalestina 420 katika kipindi cha mwezi mmoja tu uliopita wa Februari ukiwa ni muendelezo wa ukandamizaji unaofanywa na utawala huo katika ardhi unazozikalia kwa mabavu za Palestina.
Kituo cha mitaala kuhusu mateka wa Kipalestina kimetangaza katika ripoti yake ya kila mwezi kuwa mahabusu hao wanajumuisha watoto 70 na wanawake 22.
Kituo hicho aidha kimeripoti kuwa Wapalestina wengine 12 wametiwa nguvuni katika eneo lililozingirwa la Ukanda wa Gaza.

Askari wa Israel wanafanya kila aina ya jinai ikiwemo mauaji dhidi ya Wapalestina 
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, katika mwezi uliopita wa Februari mahakama za Israel zimetoa amri 88 za utiaji nguvuni wa kiidara unaoruhusu kuwaweka kizuizini Wapalestina kwa muda hadi wa miezi sita pasina kuwafungulia mashtaka.
Ripoti zinaonyesha kuwa hivi sasa kuna Wapalestina zaidi ya 6,500 wanaoshikiliwa kwenye magereza ya utawala wa Kizayuni wa Israel…/